< Mithali 28 >

1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
The wicked flee when no one pursues, but the righteous are as bold as a lion.
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
A land in rebellion has many rulers, but a man of understanding and knowledge maintains order.
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
A destitute leader who oppresses the poor is like a driving rain that leaves no food.
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
Those who forsake the law praise the wicked, but those who keep the law resist them.
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
Evil men do not understand justice, but those who seek the LORD comprehend fully.
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
Better a poor man who walks with integrity than a rich man whose ways are perverse.
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
A discerning son keeps the law, but a companion of gluttons disgraces his father.
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
He who increases his wealth by interest and usury lays it up for one who is kind to the poor.
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
Whoever turns his ear away from hearing the law, even his prayer is detestable.
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
He who leads the upright along the path of evil will fall into his own pit, but the blameless will inherit what is good.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
A rich man is wise in his own eyes, but a poor man with discernment sees through him.
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
When the righteous triumph, there is great glory, but when the wicked rise, men hide themselves.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
He who conceals his sins will not prosper, but whoever confesses and renounces them will find mercy.
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
Blessed is the man who is always reverent, but he who hardens his heart falls into trouble.
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
Like a roaring lion or a charging bear is a wicked ruler over a helpless people.
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
A leader who lacks judgment is also a great oppressor, but he who hates dishonest profit will prolong his days.
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
A man burdened by bloodguilt will flee into the Pit; let no one support him.
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
He who walks with integrity will be kept safe, but whoever is perverse in his ways will suddenly fall.
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
The one who works his land will have plenty of food, but whoever chases fantasies will have his fill of poverty.
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
A faithful man will abound with blessings, but one eager to be rich will not go unpunished.
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
To show partiality is not good, yet a man will do wrong for a piece of bread.
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
A stingy man hastens after wealth and does not know that poverty awaits him.
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
He who rebukes a man will later find more favor than one who flatters with his tongue.
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
He who robs his father or mother, saying, “It is not wrong,” is a companion to the man who destroys.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
A greedy man stirs up strife, but he who trusts in the LORD will prosper.
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
He who trusts in himself is a fool, but one who walks in wisdom will be safe.
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
Whoever gives to the poor will not be in need, but he who hides his eyes will receive many curses.
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
When the wicked come to power, people hide themselves; but when they perish, the righteous flourish.

< Mithali 28 >