< Mithali 28 >

1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
De ugudelige fly, og der er ingen, som forfølger dem; men de retfærdige ere trygge som en ung Løve.
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
Formedelst Landets Overtrædelse blive dets Fyrster mange; men iblandt Folk, der have Forstand og Kundskab, lever han længe.
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
Er han en fattig Mand, og trykker han den ringe, da bliver han som en Regn, der bortskyller, saa at der ikke bliver Brød.
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
De, som forlade Loven, rose de ugudelige; men de, som bevare Loven, strides med dem.
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
Onde Folk forstaa ikke Ret; men de, som søge Herren, forstaa alting.
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
Bedre er en fattig, som vandrer i sin Oprigtighed, end den forvendte, som vandrer paa tvende Veje, om han end er rig.
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
Den, som bevarer Loven, er en forstandig Søn; men den, som har Omgang med Fraadsere, beskæmmer sin Fader.
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
Hvo som formerer sit Gods ved Aager og Rente, samler det til at skænkes de ringe.
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
Hvo som vender sit Øre bort fra at høre Loven, endog hans Bøn er en Vederstyggelighed.
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
Hvo som leder de retsindige vild paa Ondskabs Vej, han skal falde i sin egen Grav; men de oprigtige skulle arve, hvad godt er.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
En rig Mand er viis i sine egne Øjne; men den ringe, som er forstandig, skal ransage ham.
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
Naar de retfærdige fryde sig, da er der stor Herlighed; men naar ugudelige rejse sig, skal man lede efter Folk.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
Den, som skjuler sine Overtrædelser, skal ikke have Lykke; men den, som bekender dem og afstaar fra dem, skal faa Barmhjertighed.
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
Saligt er det Menneske, som altid frygter; men den, som forhærder sit Hjerte, skal falde i Ulykke.
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
Som en brølende Løve og en omstrejfende Bjørn er den ugudelige, der hersker over et fattigt Folk.
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
En Fyrste, som fattes Forstand, er og en stor Undertrykker; men hvo der hader uretfærdig Vinding, skal forlænge sine Dage.
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
Et Menneske, betynget med en Sjæls Blod, flyr til Graven; man holde ikke paa ham.
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
Hvo som vandrer oprigtigt, skal frelses; men hvo som er forvendt og vandrer paa tvende Veje, skal falde paa een af dem.
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
Hvo som dyrker sin Jord, skal mættes af Brød; men den, som løber efter Løsgængere, skal mættes med Armod.
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
En trofast Mand skal faa mange Velsignelser; men den, som haster efter at blive rig, skal ikke kendes uskyldig.
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
Det er ikke godt at anse Personer; og dog kan en Mand forsynde sig for et Stykke Brøds Skyld.
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
En Mand med et ondt Øje haster efter Gods og ved ikke, at Mangel skal komme over ham.
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
Hvo der irettesætter et Menneske, skal derefter finde mere Gunst end den, som smigrer med Tungen.
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
Hvo der stjæler fra sin Fader eller sin Moder og siger: Det er ingen Synd, han er Stalbroder til en Ødeland.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
Den, hvis Sjæl er stolt, vækker Trætte; men den, som forlader sig paa Herren, skal blive rig.
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
Hvo som forlader sig paa sit Hjerte, han er en Daare; men den, som vandrer i Visdom, han skal reddes.
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
Hvo som giver den fattige, skal ikke have Mangel; men over den, som lukker sine Øjne til, skal der være mange Forbandelser.
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
Naar de ugudelige rejse sig, skjule Folk sig; men naar de omkomme, ville de retfærdige blive mange.

< Mithali 28 >