< Mithali 28 >

1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
惡人雖無人追趕也逃跑; 義人卻膽壯像獅子。
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
邦國因有罪過,君王就多更換; 因有聰明知識的人,國必長存。
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
窮人欺壓貧民, 好像暴雨沖沒糧食。
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
違棄律法的,誇獎惡人; 遵守律法的,卻與惡人相爭。
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
壞人不明白公義; 惟有尋求耶和華的,無不明白。
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
行為純正的窮乏人 勝過行事乖僻的富足人。
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
謹守律法的,是智慧之子; 與貪食人作伴的,卻羞辱其父。
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
人以厚利加增財物, 是給那憐憫窮人者積蓄的。
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
轉耳不聽律法的, 他的祈禱也為可憎。
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
誘惑正直人行惡道的,必掉在自己的坑裏; 惟有完全人必承受福分。
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
富足人自以為有智慧, 但聰明的貧窮人能將他查透。
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
義人得志,有大榮耀; 惡人興起,人就躲藏。
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
遮掩自己罪過的,必不亨通; 承認離棄罪過的,必蒙憐恤。
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
常存敬畏的,便為有福; 心存剛硬的,必陷在禍患裏。
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
暴虐的君王轄制貧民, 好像吼叫的獅子、覓食的熊。
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
無知的君多行暴虐; 以貪財為可恨的,必年長日久。
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
背負流人血之罪的,必往坑裏奔跑, 誰也不可攔阻他。
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
行動正直的,必蒙拯救; 行事彎曲的,立時跌倒。
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
耕種自己田地的,必得飽食; 追隨虛浮的,足受窮乏。
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
誠實人必多得福; 想要急速發財的,不免受罰。
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
看人的情面乃為不好; 人因一塊餅枉法也為不好。
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
人有惡眼想要急速發財, 卻不知窮乏必臨到他身。
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
責備人的,後來蒙人喜悅, 多於那用舌頭諂媚人的。
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
偷竊父母的,說:這不是罪, 此人就是與強盜同類。
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
心中貪婪的,挑起爭端; 倚靠耶和華的,必得豐裕。
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
心中自是的,便是愚昧人; 憑智慧行事的,必蒙拯救。
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
賙濟貧窮的,不致缺乏; 佯為不見的,必多受咒詛。
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
惡人興起,人就躲藏; 惡人敗亡,義人增多。

< Mithali 28 >