< Mithali 28 >
1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
恶人虽无人追赶也逃跑; 义人却胆壮像狮子。
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
邦国因有罪过,君王就多更换; 因有聪明知识的人,国必长存。
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
穷人欺压贫民, 好像暴雨冲没粮食。
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
违弃律法的,夸奖恶人; 遵守律法的,却与恶人相争。
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
坏人不明白公义; 惟有寻求耶和华的,无不明白。
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
行为纯正的穷乏人 胜过行事乖僻的富足人。
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
谨守律法的,是智慧之子; 与贪食人作伴的,却羞辱其父。
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
人以厚利加增财物, 是给那怜悯穷人者积蓄的。
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
转耳不听律法的, 他的祈祷也为可憎。
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
诱惑正直人行恶道的,必掉在自己的坑里; 惟有完全人必承受福分。
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
富足人自以为有智慧, 但聪明的贫穷人能将他查透。
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
义人得志,有大荣耀; 恶人兴起,人就躲藏。
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
遮掩自己罪过的,必不亨通; 承认离弃罪过的,必蒙怜恤。
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
常存敬畏的,便为有福; 心存刚硬的,必陷在祸患里。
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
暴虐的君王辖制贫民, 好像吼叫的狮子、觅食的熊。
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
无知的君多行暴虐; 以贪财为可恨的,必年长日久。
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
背负流人血之罪的,必往坑里奔跑, 谁也不可拦阻他。
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
行动正直的,必蒙拯救; 行事弯曲的,立时跌倒。
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
耕种自己田地的,必得饱食; 追随虚浮的,足受穷乏。
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
诚实人必多得福; 想要急速发财的,不免受罚。
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
看人的情面乃为不好; 人因一块饼枉法也为不好。
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
人有恶眼想要急速发财, 却不知穷乏必临到他身。
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
责备人的,后来蒙人喜悦, 多于那用舌头谄媚人的。
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
偷窃父母的,说:这不是罪, 此人就是与强盗同类。
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
心中贪婪的,挑起争端; 倚靠耶和华的,必得丰裕。
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
心中自是的,便是愚昧人; 凭智慧行事的,必蒙拯救。
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
周济贫穷的,不致缺乏; 佯为不见的,必多受咒诅。
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
恶人兴起,人就躲藏; 恶人败亡,义人增多。