< Mithali 28 >
1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
惡人無人追蹤,仍然竄逃;義人安然自得,有如雄獅。
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
由於國家的罪,領袖時有更迭;惟賴明哲之士,邦國方能久存。
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
欺壓弱小的惡霸,有如沖沒穀糧的暴雨。
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
違法的人,稱揚敗類;守法的人,與之為敵。
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
作惡的人,不明瞭正義;尋求上主的,卻全洞識。
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
為人正直的窮人,勝於行為邪僻的富人。
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
遵守法律的,是智慧之子;交結蕩子的,是取辱己父。
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
誰放貸取利增加己產,是為憐恤貧乏者積蓄。
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
對於法律,人若充耳不聞,他的祈禱,也為上主所惡。
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
勾引正直的人走上邪路的,必落在自己所掘的坑內;但正直的人仍能繼承幸福。
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
富貴的人,自認為有智慧,聰明的窮人一眼即看穿。
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
義人獲勝,群情歡騰;惡霸當道,人人走避。
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
文過飾非的,必不會順利;認錯悔改的,將蒙受憐憫。
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
常戒慎的人,必蒙祝福;心硬如鐵者,必遭災禍。
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
暴君欺凌貧窮弱小,有如咆哮怒獅,飢餓野熊。
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
無知的昏君,必橫行霸道;憎恨貪婪的,將延年益壽。
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
身負血債者,雖逃至死地,也無人搭救。
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
行走正路的,必安然無恙;愛走曲徑的,必墮入陷阱。
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
自耕其地的,必常得飽食;追求虛幻的,必飽嘗貧苦。
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
忠誠篤實的人,將滿渥福祉;急於致富的人,將難免無過。
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
顧及人的情面,原非一件好事;但為一片麵包,人卻陷身不義。
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
眼睛貪婪的人,匆匆急於致富;豈知貧乏窮困,即將臨他身上!
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
責斥他人的,終比奉承的,更得人愛戴。
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
向自己父母行竊,卻說「這並不是罪,」與強盜是同路人。
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
貪得無厭的人,必引起爭端;信賴上主的人,必心安理得。
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
自恃聰明的,實是糊塗人;行事智慧的,必安全無恙。
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
樂施濟貧的,決不會匱乏;視若無睹的,必飽受咒罵。
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
惡霸當道,人人走避;惡霸滅亡,義人興旺。