< Mithali 27 >

1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
NO te jactes del día de mañana; porque no sabes qué dará de sí el día.
2 Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
Alábete el extraño, y no tu boca; el ajeno, y no tus labios.
3 Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
Pesada es la piedra, y la arena pesa; mas la ira del necio es más pesada que ambas cosas.
4 Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
Cruel es la ira, é impetuoso el furor; mas ¿quién parará delante de la envidia?
5 Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
Mejor es reprensión manifiesta que amor oculto.
6 Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
Fieles son las heridas del que ama; pero importunos los besos del que aborrece.
7 Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
El alma harta huella el panal de miel; mas al alma hambrienta todo lo amargo es dulce.
8 Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
Cual ave que se va de su nido, tal es el hombre que se va de su lugar.
9 Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
El ungüento y el perfume alegran el corazón: y el amigo al hombre con el cordial consejo.
10 Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
No dejes á tu amigo, ni al amigo de tu padre; ni entres en casa de tu hermano el día de tu aflicción: mejor es el vecino cerca que el hermano lejano.
11 Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
Sé sabio, hijo mío, y alegra mi corazón, y tendré qué responder al que me deshonrare.
12 Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
El avisado ve el mal, [y] escóndese; [mas] los simples pasan, [y] llevan el daño.
13 vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
Quítale su ropa al que fió al extraño; y [al que fió] á la extraña, tómale prenda.
14 Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
El que bendice á su amigo en alta voz, madrugando de mañana, por maldición se le contará.
15 Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
Gotera continua en tiempo de lluvia, y la mujer rencillosa, son semejantes:
16 kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
El que pretende contenerla, arresta el viento: ó el aceite en su mano derecha.
17 Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
Hierro con hierro se aguza; y el hombre aguza el rostro de su amigo.
18 Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
El que guarda la higuera, comerá su fruto; y el que guarda á su señor, será honrado.
19 Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
Como un agua se parece á otra, así el corazón del hombre al otro.
20 Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
El sepulcro y la perdición nunca se hartan: así los ojos del hombre nunca están satisfechos. (Sheol h7585)
21 Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
El crisol [prueba] la plata, y la hornaza el oro: y al hombre la boca del que lo alaba.
22 Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
Aunque majes al necio en un mortero entre granos de trigo á pisón majados, no se quitará de él su necedad.
23 Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
Considera atentamente el aspecto de tus ovejas; pon tu corazón á tus rebaños:
24 maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
Porque las riquezas no son para siempre; ¿y [será] la corona para perpetuas generaciones?
25 Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
Saldrá la grama, aparecerá la hierba, y segaránse las hierbas de los montes.
26 Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
Los corderos para tus vestidos, y los cabritos para el precio del campo:
27 Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.
Y abundancia de leche de las cabras para tu mantenimiento, y para mantenimiento de tu casa, y para sustento de tus criadas.

< Mithali 27 >