< Mithali 27 >

1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
ne glorieris in crastinum ignorans quid superventura pariat dies
2 Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
laudet te alienus et non os tuum extraneus et non labia tua
3 Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
grave est saxum et onerosa harena sed ira stulti utroque gravior
4 Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
ira non habet misericordiam nec erumpens furor et impetum concitati ferre quis poterit
5 Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
melior est manifesta correptio quam amor absconditus
6 Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
meliora sunt vulnera diligentis quam fraudulenta odientis oscula
7 Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
anima saturata calcabit favum anima esuriens et amarum pro dulce sumet
8 Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
sicut avis transmigrans de nido suo sic vir qui relinquit locum suum
9 Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
unguento et variis odoribus delectatur cor et bonis amici consiliis anima dulcoratur
10 Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
amicum tuum et amicum patris tui ne dimiseris et domum fratris tui ne ingrediaris in die adflictionis tuae melior est vicinus iuxta quam frater procul
11 Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
stude sapientiae fili mi et laetifica cor meum ut possim exprobranti respondere sermonem
12 Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
astutus videns malum absconditus est parvuli transeuntes sustinuere dispendia
13 vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
tolle vestimentum eius qui spopondit pro extraneo et pro alienis auferto pignus
14 Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
qui benedicit proximo suo voce grandi de nocte consurgens maledicenti similis erit
15 Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
tecta perstillantia in die frigoris et litigiosa mulier conparantur
16 kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
qui retinet eam quasi qui ventum teneat et oleum dexterae suae vocabit
17 Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
ferrum ferro acuitur et homo exacuit faciem amici sui
18 Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
qui servat ficum comedet fructus eius et qui custos est domini sui glorificabitur
19 Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
quomodo in aquis resplendent vultus prospicientium sic corda hominum manifesta sunt prudentibus
20 Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
infernus et perditio non replentur similiter et oculi hominum insatiabiles (Sheol h7585)
21 Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
quomodo probatur in conflatorio argentum et in fornace aurum sic probatur homo ore laudantis
22 Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
si contuderis stultum in pila quasi tisanas feriente desuper pilo non auferetur ab eo stultitia eius
23 Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
diligenter agnosce vultum pecoris tui tuosque greges considera
24 maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
non enim habebis iugiter potestatem sed corona tribuetur in generatione generationum
25 Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
aperta sunt prata et apparuerunt herbae virentes et collecta sunt faena de montibus
26 Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
agni ad vestimentum tuum et hedi agri pretium
27 Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.
sufficiat tibi lac caprarum in cibos tuos in necessaria domus tuae et ad victum ancillis tuis

< Mithali 27 >