< Mithali 27 >
1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
Ne glorieris in crastinum, ignorans quid superventura pariat dies.
2 Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
Laudet te alienus, et non os tuum: extraneus, et non labia tua.
3 Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
Grave est saxum, et onerosa arena: sed ira stulti utroque gravior.
4 Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
Ira non habet misericordiam, nec erumpens furor: et impetum concitati spiritus ferre quis poterit?
5 Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
Melior est manifesta correptio, quam amor absconditus.
6 Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
Meliora sunt vulnera diligentis, quam fraudulenta oscula odientis
7 Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
Anima saturata calcabit favum: et anima esuriens etiam amarum pro dulci sumet.
8 Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
Sicut avis transmigrans de nido suo, sic vir qui derelinquit locum suum.
9 Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
Unguento et variis odoribus delectatur cor: et bonis amici consiliis anima dulcoratur.
10 Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
Amicum tuum, et amicum patris tui ne dimiseris: et domum fratris tui ne ingrediaris in die afflictionis tuae. Melior est vicinus iuxta, quam frater procul.
11 Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
Stude sapientiae fili mi, et laetifica cor meum, ut possim exprobranti respondere sermonem.
12 Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
Astutus videns malum, absconditus est: parvuli transeuntes sustinuerunt dispendia.
13 vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
Tolle vestimentum eius, qui spopondit pro extraneo: et pro alienis, aufer ei pignus.
14 Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
Qui benedicit proximo suo voce grandi, de nocte consurgens maledicenti similis erit.
15 Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
Tecta perstillantia in die frigoris, et litigiosa mulier comparantur:
16 kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
qui retinet eam, quasi qui ventum teneat, et oleum dexterae suae evacuabit.
17 Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
Ferrum ferro exacuitur, et homo exacuit faciem amici sui.
18 Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
Qui servat ficum, comedet fructus eius: et qui custos est domini sui, glorificabitur.
19 Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
Quomodo in aquis resplendent vultus prospicientium, sic corda hominum manifesta sunt prudentibus.
20 Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol )
Infernus et perditio numquam implentur: similiter et oculi hominum insatiabiles: (Sheol )
21 Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
Quomodo probatur in conflatorio argentum, et in fornace aurum: sic probatur homo ore laudantis. Cor iniqui inquirit mala, cor autem rectum inquirit scientiam.
22 Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
Si contuderis stultum in pila quasi ptisanas feriente desuper pilo, non auferetur ab eo stultitia eius.
23 Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
Diligenter agnosce vultum pecoris tui, tuosque greges considera:
24 maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
Non enim habebis iugiter potestatem: sed corona tribuetur in generatione et generationem.
25 Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
Aperta sunt prata, et apparuerunt herbae virentes, et collecta sunt foena de montibus.
26 Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
Agni ad vestimentum tuum: et hoedi, agri pretium.
27 Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.
Sufficiat tibi lac caprarum in cibos tuos, et in necessaria domus tuae: et ad victum ancillis tuis.