< Mithali 27 >

1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
Ne te félicite pas du jour de demain, car tu ne sais ce que peut apporter chaque jour.
2 Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
Qu’un autre fasse ton éloge et non ta propre bouche; un étrangers et non tes lèvres à toi.
3 Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
Lourde est la pierre, pesant le sable; mais le dépit d’un sot pèse plus lourd que les deux.
4 Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
Cruelle est la colère, violent le courroux; mais qui peut tenir devant la jalousie?
5 Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
Mieux vaut une réprimande ouverte qu’une amitié qui se dérobe.
6 Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
Les blessures faites par un ami sont preuve d’affection, un ennemi est prodigue de caresses.
7 Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
La satiété fait fi du miel; la faim trouve doux ce qui est amer.
8 Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
Comme l’oiseau qui erre loin de son nid, tel est l’homme qui erre loin de son pays.
9 Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
Huile et parfum réjouissent le cœur; de même la bonté suave d’un ami qui donne de sincères conseils.
10 Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
N’Abandonne ni ton ami ni l’ami de ton père, ne franchis pas le seuil de ton frère au jour de ton malheur; mieux vaut un voisin qui est près de toi qu’un frère qui se tient à l’écart.
11 Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
Sois sage, mon fils, tu réjouiras mon cœur, et j’aurai de quoi répliquer à qui m’insulte.
12 Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
L’Homme avisé aperçoit le danger et se met à l’abri; les niais passent outre et en pâtissent.
13 vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
Il s’est porté garant pour un autre: saisis son vêtement; il a cautionné une étrangère: nantis-toi de son gage!
14 Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
Assourdir de grand matin son prochain par de bruyants saluts, c’est comme si on lui disait des injures.
15 Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
Une gouttière qui se déverse par un jour d’orage et une femme acariâtre, c’est tout un.
16 kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
Vouloir la retenir, c’est retenir le vent ou recueillir de l’huile dans sa main.
17 Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
Le fer devient poli au contact du fer et l’homme au contact de son prochain.
18 Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
Qui veille sur le figuier jouira de ses fruits qui veine sur son maître recueillera de l’honneur.
19 Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
Comme dans l’eau le visage répond au visage, ainsi chez les hommes les cœurs se répondent.
20 Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
Cheol et abîme sont insatiables; les yeux de l’homme le sont également. (Sheol h7585)
21 Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
La fournaise, pour l’argent, le creuset pour l’or, et l’homme est prisé d’après sa réputation.
22 Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
Tu broierais le sot dans un mortier avec le pilon, comme on fait des graines, que sa sottise ne se détacherait pas de lui.
23 Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
Tâche de bien connaître l’état de tes brebis, porte ton attention sur tes troupeaux.
24 maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
Car les biens ne dureront pas toujours: les dignités se transmettent-elles de génération en génération?
25 Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
Que la végétation se fasse jour, que la verdure apparaisse, que les herbes des hauteurs soient recueillies,
26 Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
et tu auras des brebis pour te vêtir, des béliers pour payer le prix d’un champ,
27 Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.
du lait de chèvres en abondance, pour te nourrir toi et ta famille et faire vivre tes domestiques.

< Mithali 27 >