< Mithali 27 >

1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
Ne vous vantez pas du lendemain; car vous ne savez pas ce qu'un jour peut apporter.
2 Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
Qu'un autre homme te loue, et pas votre propre bouche; un étranger, et non vos propres lèvres.
3 Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
Une pierre est lourde, et le sable est un fardeau; mais la provocation d'un idiot est plus lourde que les deux.
4 Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
La colère est cruelle, et la colère est écrasante; mais qui est capable de résister à la jalousie?
5 Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
Mieux vaut une réprimande ouverte que l'amour caché.
6 Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
Les blessures d'un ami sont fidèles, bien que les baisers d'un ennemi soient profonds.
7 Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
Une âme rassasiée a horreur du rayon de miel; mais pour une âme affamée, toute chose amère est douce.
8 Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
Comme un oiseau qui s'éloigne de son nid, ainsi est un homme qui erre loin de sa maison.
9 Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
Le parfum et l'encens apportent de la joie au cœur; tout comme les conseils sérieux de l'ami d'un homme.
10 Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
N'abandonne pas ton ami et l'ami de ton père. N'allez pas chez votre frère le jour de votre catastrophe. Un voisin proche vaut mieux qu'un frère éloigné.
11 Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
Sois sage, mon fils, et apporte la joie dans mon cœur, alors je pourrai répondre à mon tourmenteur.
12 Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
L'homme prudent voit le danger et se réfugie; mais les simples passent, et en souffrent.
13 vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
Prenez son vêtement quand il met en gage un étranger. Tenez-le pour une femme rebelle!
14 Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
Celui qui bénit son prochain avec une voix forte, tôt le matin, il sera pris comme une malédiction par lui.
15 Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
Une goutte continue un jour de pluie et une épouse contestataire se ressemblent:
16 kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
La retenir, c'est comme retenir le vent, ou comme de saisir de l'huile dans sa main droite.
17 Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
Le fer aiguise le fer; ainsi un homme aiguise le visage de son ami.
18 Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
Celui qui soigne le figuier mangera son fruit. Celui qui s'occupe de son maître sera honoré.
19 Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
Comme l'eau reflète un visage, donc le cœur d'un homme reflète l'homme.
20 Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
Sheol et Abaddon ne sont jamais satisfaits; et les yeux d'un homme ne sont jamais satisfaits. (Sheol h7585)
21 Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
Le creuset est pour l'argent, et le fourneau pour l'or; mais l'homme est raffiné par ses louanges.
22 Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
Bien que tu broies un fou dans un mortier avec un pilon, avec le grain, mais sa folie ne lui sera pas enlevée.
23 Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
Connaissez bien l'état de vos troupeaux, et faites attention à vos troupeaux,
24 maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
car les richesses ne sont pas éternelles, et la couronne ne perdure pas à travers les générations.
25 Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
On enlève le foin, et la nouvelle pousse apparaît, les herbes des collines sont rassemblées.
26 Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
Les agneaux servent à te vêtir, et les chèvres sont le prix d'un champ.
27 Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.
Il yaura du lait de chèvre en abondance pour votre nourriture, pour la nourriture de votre famille, et pour la nourriture de vos servantes.

< Mithali 27 >