< Mithali 27 >

1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
Boast not thyself of tomorrow, for thou know not what a day may bring forth.
2 Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
Let another man praise thee, and not thine own mouth, a stranger, and not thine own lips.
3 Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
A stone is heavy, and the sand weighty, but a fool's vexation is heavier than both.
4 Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
Wrath is cruel, and anger is overwhelming, but who is able to stand before jealousy?
5 Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
Better is open rebuke than love that is hidden.
6 Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
Faithful are the wounds of a friend, but the kisses of an enemy are profuse.
7 Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
The full soul loathes a honeycomb, but to the hungry soul every bitter thing is sweet.
8 Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
As a bird that wanders from her nest, so is a man who wanders from his place.
9 Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
Oil and perfume rejoice the heart, so too the sweetness of a man's friend by hearty counsel.
10 Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
Forsake not thine own friend, and thy father's friend. And go not to thy brother's house in the day of thy calamity. Better is a neighbor nearby than a brother far off.
11 Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
My son, be wise, and make my heart glad, that I may answer him who reproaches me.
12 Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
A prudent man sees the evil, and hides himself. The simple pass on, and suffer for it.
13 vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
Take his garment who is surety for a stranger, and hold him in pledge who is surety for a strange woman.
14 Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
He who blesses his friend with a loud voice, rising early in the morning, it shall be considered a curse to him.
15 Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
A continual dropping in a very rainy day, and a contentious woman are alike.
16 kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
He who would restrain her restrains the wind, and his right hand encounters oil.
17 Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
Iron sharpens iron, so a man sharpens the countenance of his friend.
18 Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
He who keeps the fig tree shall eat the fruit of it, and he who regards his master shall be honored.
19 Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
As in water face is to face, so the heart of a man is to a man.
20 Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
Sheol and Abaddon are never satisfied, and the eyes of man are never satisfied. (Sheol h7585)
21 Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
The refining pot is for silver, and the furnace for gold, and a man is tried by his praise.
22 Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
Though thou should pound a fool in a mortar with a pestle along with crushed grain, yet his foolishness will not depart from him.
23 Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
Be thou diligent to know the state of thy flocks, and look well to thy herds.
24 maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
For riches are not forever. And does the crown endure to all generations?
25 Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
The hay is carried, and the tender grass shows itself, and the herbs of the mountains are gathered in.
26 Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
The lambs are for thy clothing, and the goats are the cost of the field.
27 Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.
And then will be goats' milk enough for thy food; for the food of thy household, and maintenance for thy maidens.

< Mithali 27 >