< Mithali 27 >
1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
Ne hvali se danom sutrašnjim jer ne znaš što danas može donijeti.
2 Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
Neka te hvali drugi, a ne tvoja usta, tuđinac, a ne tvoje usne.
3 Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
Težak je kamen i pijesak je težak, ali je od obojega teži bezumnikov bijes.
4 Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
Jarost je okrutna i srdžba žestoka a tko će odoljeti ljubomoru?
5 Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
Bolji je javni ukor nego lažna ljubav.
6 Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
Čestiti su udarci prijateljevi, a lažni poljupci neprijateljevi.
7 Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
Sito grlo prezire i med samotok, a gladnu je i sve gorko - slatko.
8 Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
Kao ptica daleko od gnijezda svog, takav je čovjek daleko od svojeg zavičaja.
9 Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
Kao što ulje i kad vesele srce, tako i slatkoća prijateljstva tješi dušu.
10 Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
Ne ostavljaj prijatelja svoga ni prijatelja očeva i ne dolazi u kuću bratovu kad si u nesreći; bolji je susjed blizu nego brat daleko.
11 Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
Budi mudar, sine moj, i obraduj mi srce da mogu odgovoriti onome koji me grdi.
12 Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
Pametan čovjek opazi zlo i skrije se, a glupaci idu bezbrižno i trpe kaznu.
13 vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
Uzmi haljinu onomu tko je jamčio za drugoga i oplijeni ga mjesto tuđinca.
14 Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
Tko pozdravlja svoga prijatelja naglas, a rano ujutro, prima mu se blagoslov za kletvu.
15 Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
Streha što prokišnjava za žestoke kiše i svadljiva žena - jedno su te isto.
16 kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
Tko nju zaustavlja, zaustavlja vjetar i desnicom hvata ulje.
17 Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
Željezo se željezom oštri i čovjek oštri jedan drugoga.
18 Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
Tko čuva smokvu, jede od njena ploda, i tko čuva svoga gospodara, poštiva se.
19 Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
Kao što se u vodi različito odražava lice od lica, tako i u srcu čovjek od čovjeka.
20 Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol )
Carstvo Smrti i Propast ne mogu se zasititi, tako ni oči čovječje. (Sheol )
21 Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
Taljika je za srebro i peć za zlato, a čovjek se poznaje po ustima koja ga hvale.
22 Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
Da bezumnika stučeš tučkom u stupi, ne bi ga ostavila ludost njegova.
23 Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
Brižno pazi na stoku svoju i srcem se brini o stadima,
24 maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
jer blago ne traje dovijeka; i baštini li se kruna od koljena do koljena?
25 Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
Kad trava nikne i zelen se pokaže i bilje se kupi planinsko,
26 Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
tad su ti janjci za odijelo i jarci za kupovinu polja;
27 Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.
tad imaš izobilje kozjega mlijeka sebi za jelo, i za hranu kući svojoj i za prehranu sluškinjama svojim.