< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
quomodo nix aestate et pluvia in messe sic indecens est stulto gloria
2 Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
sicut avis ad alia transvolans et passer quolibet vadens sic maledictum frustra prolatum in quempiam superveniet
3 Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
flagellum equo et camus asino et virga dorso inprudentium
4 Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
ne respondeas stulto iuxta stultitiam suam ne efficiaris ei similis
5 Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
responde stulto iuxta stultitiam suam ne sibi sapiens esse videatur
6 Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
claudus pedibus et iniquitatem bibens qui mittit verba per nuntium stultum
7 Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
quomodo pulchras frustra habet claudus tibias sic indecens est in ore stultorum parabola
8 Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
sicut qui mittit lapidem in acervum Mercurii ita qui tribuit insipienti honorem
9 Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
quomodo si spina nascatur in manu temulenti sic parabola in ore stultorum
10 Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
iudicium determinat causas et qui inponit stulto silentium iras mitigat
11 Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
sicut canis qui revertitur ad vomitum suum sic inprudens qui iterat stultitiam suam
12 Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
vidisti hominem sapientem sibi videri magis illo spem habebit stultus
13 Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
dicit piger leaena in via leo in itineribus
14 Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
sicut ostium vertitur in cardine suo ita piger in lectulo suo
15 Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
abscondit piger manus sub ascellas suas et laborat si ad os suum eas converterit
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
sapientior sibi piger videtur septem viris loquentibus sententias
17 Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
sicut qui adprehendit auribus canem sic qui transit et inpatiens commiscetur rixae alterius
18 Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
sicut noxius est qui mittit lanceas et sagittas et mortem
19 ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
sic vir qui fraudulenter nocet amico suo et cum fuerit deprehensus dicit ludens feci
20 Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
cum defecerint ligna extinguetur ignis et susurrone subtracto iurgia conquiescunt
21 Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
sicut carbones ad prunam et ligna ad ignem sic homo iracundus suscitat rixas
22 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
verba susurronis quasi simplicia et ipsa perveniunt ad intima ventris
23 Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
quomodo si argento sordido ornare velis vas fictile sic labia tumentia cum pessimo corde sociata
24 Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
labiis suis intellegitur inimicus cum in corde tractaverit dolos
25 Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
quando submiserit vocem suam ne credideris ei quoniam septem nequitiae sunt in corde illius
26 Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
qui operit odium fraudulenter revelabitur malitia eius in concilio
27 Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
qui fodit foveam incidet in eam et qui volvit lapidem revertetur ad eum
28 Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.
lingua fallax non amat veritatem et os lubricum operatur ruinas

< Mithali 26 >