< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
夏天落雪,收割时下雨,都不相宜; 愚昧人得尊荣也是如此。
2 Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
麻雀往来,燕子翻飞; 这样,无故的咒诅也必不临到。
3 Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
鞭子是为打马,辔头是为勒驴; 刑杖是为打愚昧人的背。
4 Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
不要照愚昧人的愚妄话回答他, 恐怕你与他一样。
5 Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
要照愚昧人的愚妄话回答他, 免得他自以为有智慧。
6 Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
借愚昧人手寄信的, 是砍断自己的脚,自受损害。
7 Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
瘸子的脚空存无用; 箴言在愚昧人的口中也是如此。
8 Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
将尊荣给愚昧人的, 好像人把石子包在机弦里。
9 Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
箴言在愚昧人的口中, 好像荆棘刺入醉汉的手。
10 Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
雇愚昧人的,与雇过路人的, 就像射伤众人的弓箭手。
11 Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
愚昧人行愚妄事,行了又行, 就如狗转过来吃它所吐的。
12 Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
你见自以为有智慧的人吗? 愚昧人比他更有指望。
13 Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
懒惰人说:道上有猛狮, 街上有壮狮。
14 Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
门在枢纽转动, 懒惰人在床上也是如此。
15 Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
懒惰人放手在盘子里, 就是向口撤回也以为劳乏。
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
懒惰人看自己比七个善于应对的人更有智慧。
17 Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
过路被事激动,管理不干己的争竞, 好像人揪住狗耳。
18 Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
人欺凌邻舍,却说: 我岂不是戏耍吗? 他就像疯狂的人抛掷火把、利箭, 与杀人的兵器。
19 ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
20 Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
火缺了柴就必熄灭; 无人传舌,争竞便止息。
21 Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
好争竞的人煽惑争端, 就如余火加炭,火上加柴一样。
22 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
传舌人的言语,如同美食, 深入人的心腹。
23 Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
火热的嘴,奸恶的心, 好像银渣包的瓦器。
24 Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
怨恨人的,用嘴粉饰, 心里却藏着诡诈;
25 Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
他用甜言蜜语,你不可信他, 因为他心中有七样可憎恶的。
26 Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
他虽用诡诈遮掩自己的怨恨, 他的邪恶必在会中显露。
27 Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
挖陷坑的,自己必掉在其中; 滚石头的,石头必反滚在他身上。
28 Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.
虚谎的舌恨他所压伤的人; 谄媚的口败坏人的事。

< Mithali 26 >