< Mithali 25 >

1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
To również są przysłowia Salomona, które przepisali mężowie Ezechiasza, króla Judy.
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
Chwałą Boga jest sprawę taić, ale chwałą królów – dociekać sprawy.
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
Wysokość niebios i głębia ziemi, i serca królów są niezbadane.
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
Usuń żużel ze srebra, a wyjdzie naczynie dla złotnika.
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
Usuń niegodziwego sprzed króla, a jego tron umocni się w sprawiedliwości.
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
Nie wywyższaj się przed królem i nie stawaj na miejscu wielkich;
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
Bo lepiej, żeby ci powiedziano: Podejdź tu, niż żeby cię poniżono przed księciem, którego twoje oczy widziały.
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
Nie spiesz się do kłótni, bo na końcu [nie będziesz wiedział], co zrobić, gdy cię zawstydzi twój bliźni.
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
Załatw sprawę ze swoim bliźnim i nie zdradzaj tajemnicy drugiemu;
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
By ten, który słucha, nie zawstydził cię, a twoja niesława nie przylgnęła do ciebie.
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
Odpowiednio wypowiedziane słowo [jest jak] złote jabłko w srebrnych rzeźbach.
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
Jak złoty kolczyk i klejnot ze szczerego złota tak jest dla uszu posłusznego ten, który mądrze strofuje.
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
Czym chłód śniegu w czasie żniwa, [tym] wierny posłaniec dla tych, którzy go posyłają, bo pokrzepia dusze swych panów.
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
Człowiek, który się chlubi zmyślonym darem, jest jak chmury i wiatr bez deszczu.
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
Cierpliwością można przekonać władcę, a łagodny język łamie kości.
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
Czy znalazłeś miód? Zjedz tyle, ile trzeba, byś objadłszy się, nie zwrócił go.
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
Oddal nogę od domu bliźniego, by nie miał cię dość i cię nie znienawidził.
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
Kto mówi fałszywe świadectwo przeciw swemu bliźniemu, [jest] młotem i mieczem, i ostrą strzałą.
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
Ufność w człowieka niewiernego w dniu ucisku jest [jak] złamany ząb i zwichnięta noga.
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
[Jak] ten, kto zabiera odzienie w czasie zimy i jak ocet na saletrze taki [jest ten], kto śpiewa pieśni smutnemu sercu.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
Jeśli twój nieprzyjaciel jest głodny, nakarm go chlebem, a jeśli jest spragniony, napój go wodą;
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
Bo zgarniesz rozżarzone węgle na jego głowę, a PAN cię nagrodzi.
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
[Jak] północny wiatr przepędza deszcz, tak gniewna twarz [przepędza] plotkarski język.
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
Lepiej mieszkać w kącie pod dachem niż z kłótliwą żoną w przestronnym domu.
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
[Jak] zimna woda dla pragnącej duszy, [tak] dobra wieść z dalekiej ziemi.
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
[Jak] zmącone źródło i zepsuty zdrój, [tak] sprawiedliwy, który upada przed niegodziwym.
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
Niedobrze jest jeść za dużo miodu, a szukanie własnej chwały nie jest chwałą.
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
Człowiek, który nie panuje nad swoim duchem, jest [jak] miasto zburzone [i] bez muru.

< Mithali 25 >