< Mithali 25 >

1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
haec quoque parabolae Salomonis quas transtulerunt viri Ezechiae regis Iuda
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
gloria Dei celare verbum et gloria regum investigare sermonem
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
caelum sursum et terra deorsum et cor regum inscrutabile
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
aufer robiginem de argento et egredietur vas purissimum
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
aufer impietatem de vultu regis et firmabitur iustitia thronus eius
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
ne gloriosus appareas coram rege et in loco magnorum ne steteris
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
melius est enim ut dicatur tibi ascende huc quam ut humilieris coram principe
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
quae viderunt oculi tui ne proferas in iurgio cito ne postea emendare non possis cum dehonestaveris amicum tuum
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
causam tuam tracta cum amico tuo et secretum extraneo non reveles
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
ne forte insultet tibi cum audierit et exprobrare non cesset
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
mala aurea in lectis argenteis qui loquitur verbum in tempore suo
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
inauris aurea et margaritum fulgens qui arguit sapientem et aurem oboedientem
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
sicut frigus nivis in die messis ita legatus fidelis ei qui misit eum animam illius requiescere facit
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
nubes et ventus et pluviae non sequentes vir gloriosus et promissa non conplens
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
patientia lenietur princeps et lingua mollis confringet duritiam
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
mel invenisti comede quod sufficit tibi ne forte saturatus evomas illud
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
subtrahe pedem tuum de domo proximi tui nequando satiatus oderit te
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
iaculum et gladius et sagitta acuta homo qui loquitur contra proximum suum testimonium falsum
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
dens putridus et pes lapsus qui sperat super infideli in die angustiae
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
et amittit pallium in die frigoris acetum in nitro et qui cantat carmina cordi pessimo
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
si esurierit inimicus tuus ciba illum et si sitierit da ei aquam bibere
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
prunam enim congregabis super caput eius et Dominus reddet tibi
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
ventus aquilo dissipat pluvias et facies tristis linguam detrahentem
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
melius est sedere in angulo domatis quam cum muliere litigiosa et in domo communi
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
aqua frigida animae sitienti et nuntius bonus de terra longinqua
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
fons turbatus pede et vena corrupta iustus cadens coram impio
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
sicut qui mel multum comedit non est ei bonum sic qui scrutator est maiestatis opprimitur gloria
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
sicut urbs patens et absque murorum ambitu ita vir qui non potest in loquendo cohibere spiritum suum

< Mithali 25 >