< Mithali 25 >

1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
גם-אלה משלי שלמה-- אשר העתיקו אנשי חזקיה מלך-יהודה
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
כבד אלהים הסתר דבר וכבד מלכים חקר דבר
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
שמים לרום וארץ לעמק ולב מלכים אין חקר
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
הגו סיגים מכסף ויצא לצרף כלי
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
הגו רשע לפני-מלך ויכון בצדק כסאו
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
אל-תתהדר לפני-מלך ובמקום גדלים אל-תעמד
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
כי טוב אמר-לך עלה-הנה מהשפילך לפני נדיב--אשר ראו עיניך
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
אל-תצא לרב מהר פן מה-תעשה באחריתה--בהכלים אתך רעך
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
ריבך ריב את-רעך וסוד אחר אל-תגל
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
פן-יחסדך שמע ודבתך לא תשוב
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
תפוחי זהב במשכיות כסף-- דבר דבר על-אפניו
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
נזם זהב וחלי-כתם-- מוכיח חכם על-אזן שמעת
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
כצנת שלג ביום קציר--ציר נאמן לשלחיו ונפש אדניו ישיב
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
נשיאים ורוח וגשם אין-- איש מתהלל במתת-שקר
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
בארך אפים יפתה קצין ולשון רכה תשבר-גרם
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
דבש מצאת אכל דיך פן-תשבענו והקאתו
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
הקר רגלך מבית רעך פן-ישבעך ושנאך
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
מפיץ וחרב וחץ שנון-- איש ענה ברעהו עד שקר
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
שן רעה ורגל מועדת-- מבטח בוגד ביום צרה
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
מעדה-בגד ביום קרה--חמץ על-נתר ושר בשרים על לב-רע
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
אם-רעב שנאך האכלהו לחם ואם-צמא השקהו מים
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
כי גחלים--אתה חתה על-ראשו ויהוה ישלם-לך
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
רוח צפון תחולל גשם ופנים נזעמים לשון סתר
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
טוב שבת על-פנת-גג-- מאשת מדונים (מדינים) ובית חבר
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
מים קרים על-נפש עיפה ושמועה טובה מארץ מרחק
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
מעין נרפש ומקור משחת-- צדיק מט לפני-רשע
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
אכל דבש הרבות לא-טוב וחקר כבדם כבוד
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
עיר פרוצה אין חומה-- איש אשר אין מעצר לרוחו

< Mithali 25 >