< Mithali 25 >
1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
Also these ben the Parablis of Salomon, whiche the men of Ezechie, kyng of Juda, translatiden.
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
The glorie of God is to hele a word; and the glorie of kyngis is to seke out a word.
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
Heuene aboue, and the erthe bynethe, and the herte of kyngis is vnserchable.
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
Do thou a wei rust fro siluer, and a ful cleene vessel schal go out.
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
Do thou awei vnpite fro the cheer of the kyng, and his trone schal be maad stidfast bi riytfulnesse.
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
Appere thou not gloriouse bifore the kyng, and stonde thou not in the place of grete men.
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
For it is betere, that it be seid to thee, Stie thou hidur, than that thou be maad low bifore the prince.
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
Brynge thou not forth soone tho thingis in strijf, whiche thin iyen sien; lest aftirward thou maist not amende, whanne thou hast maad thi frend vnhonest.
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
Trete thi cause with thi frend, and schewe thou not priuyte to a straunge man;
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
lest perauenture he haue ioye of thi fal, whanne he hath herde, and ceesse not to do schenschipe to thee. Grace and frenschip delyueren, whiche kepe thou to thee, that thou be not maad repreuable.
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
A goldun pomel in beddis of siluer is he, that spekith a word in his time.
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
A goldun eere ryng, and a schinynge peerle is he, that repreueth a wijs man, and an eere obeiynge.
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
As the coold of snow in the dai of heruest, so a feithful messanger to hym that sente `thilke messanger, makith his soule to haue reste.
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
A cloude and wind, and reyn not suynge, is a gloriouse man, and not fillynge biheestis.
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
A prince schal be maad soft bi pacience; and a soft tunge schal breke hardnesse.
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
Thou hast founde hony, ete thou that that suffisith to thee; lest perauenture thou be fillid, and brake it out.
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
Withdrawe thi foot fro the hous of thi neiybore; lest sum tyme he be fillid, and hate thee.
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
A dart, and a swerd, and a scharp arowe, a man that spekith fals witnessing ayens his neiybore.
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
A rotun tooth, and a feynt foot is he, that hopith on an vnfeithful man in the dai of angwisch,
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
and leesith his mentil in the dai of coold. Vynegre in a vessel of salt is he, that singith songis to the worste herte. As a mouyte noieth a cloth, and a worm noieth a tree, so the sorewe of a man noieth the herte.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
If thin enemy hungrith, feede thou him; if he thirstith, yyue thou watir to hym to drinke;
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
for thou schalt gadere togidere coolis on his heed; and the Lord schal yelde to thee.
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
The north wind scatereth reynes; and a sorewful face distrieth a tunge bacbitinge.
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
It is betere to sitte in the corner of an hous without roof, than with a womman ful of chidyng, and in a comyn hous.
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
Coold watir to a thirsti man; and a good messanger fro a fer lond.
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
A welle disturblid with foot, and a veyne brokun, a iust man fallinge bifore a wickid man.
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
As it is not good to hym that etith myche hony; so he that is a serchere of maieste, schal be put doun fro glorie.
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
As a citee opyn, and with out cumpas of wallis; so is a man that mai not refreyne his spirit in speking.