< Mithali 25 >

1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
These also are proverbs of Solomon, which the men of Hezekiah, king of Judah, collected.
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
It is the glory of God to conceal a thing; But it is the glory of kings to search out a matter.
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
As the heavens for their height, And as the earth for its depth, So is the heart of kings unsearchable!
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
Take away the dross from the silver, And there will come forth a vessel for the founder;
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
Take away the wicked man from the presence of the king, And his throne will be established by righteousness.
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
Put not thyself forth in the presence of the king, Nor set thyself in the place of the great;
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
For better is it that one should say to thee, “Come up hither!” Than that he should put thee in a lower place, In the presence of the prince whom thine eyes behold.
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
Go not forth hastily to engage in a suit, Lest thou know not what to do in the end of it, When thine adversary hath put thee to shame.
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
Maintain thy cause with thine adversary, But reveal not another's secret;
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
Lest he that heareth it put thee to shame, And thy infamy depart not from thee.
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
A word spoken in season Is like apples of gold in figured-work of silver.
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
As a ring of gold, and an ornament of fine gold, So is a wise reprover to an attentive ear.
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
As the cold of snow in the time of harvest, So is a faithful messenger to them that send him; For he refresheth the spirit of his masters.
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
As clouds and wind without rain, So is the man that boasteth falsely of giving.
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
By long forbearing is a prince appeased; And a soft tongue breaketh bones.
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
Hast thou found honey? eat what is sufficient for thee, Lest thou be surfeited with it, and vomit it up.
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
Let thy foot be seldom in the house of thy friend, Lest he be surfeited with thee and hate thee.
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
A battle-hammer, and a sword, and a sharp arrow, Is the man who beareth false witness against his neighbor.
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
As a broken tooth, and a wavering foot, So is trust in an unfaithful man in time of trouble.
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
As he that taketh off a garment on a cold day, As vinegar upon nitre, So is he that singeth songs to a heavy heart.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
If thine enemy be hungry, give him bread to eat; And if he be thirsty, give him water to drink;
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
For thou wilt heap coals of fire upon his head, And the LORD will reward thee.
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
As the north wind bringeth forth rain, So a backbiting tongue maketh an angry countenance.
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
Better is it to dwell in a corner of the housetop, Than with a quarrelsome woman in a large house.
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
As cold water to the thirsty, So is good news from a far country.
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
As a troubled fountain, and as a corrupted spring, So is a righteous man falling before the wicked.
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
To eat much honey is not good; So the search of high things is weariness.
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
As a city broken through and without a wall, So is he that hath no rule over his spirit.

< Mithali 25 >