< Mithali 25 >
1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
These are also proverbs of Solomon, which the men of Hezekiah king of Judah copied out.
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
It is the glory of God to conceal a thing: but the honour of kings is to search out a matter.
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
The heaven for height, and the earth for depth, and the heart of kings is unsearchable.
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
Take away the dross from the silver, and there shall come forth a vessel for the finer.
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
Take away the wicked from before the king, and his throne shall be established in righteousness.
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
Put not forth yourself in the presence of the king, and stand not in the place of great men:
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
For better it is that it be said unto you, Come up here; than that you should be put lower in the presence of the prince whom your eyes have seen.
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
Go not forth hastily to strive, lest you know not what to do in the end thereof, when your neighbour has put you to shame.
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
Debate your cause with your neighbour himself; and discover not a secret to another:
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
Lest he that hears it put you to shame, and your ill repute turn not away.
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
A word fitly spoken is like apples of gold in pictures of silver.
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
As an earring of gold, and an ornament of fine gold, so is a wise reprover upon an obedient ear.
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
As the cold of snow in the time of harvest, so is a faithful messenger to them that send him: for he refreshes the soul of his masters.
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
Whoso boasts himself of a false gift is like clouds and wind without rain.
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
By long forbearing is a prince persuaded, and a soft tongue breaks the bone.
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
Have you found honey? eat so much as is sufficient for you, lest you be filled therewith, and vomit it.
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
Withdraw your foot from your neighbour's house; lest he be weary of you, and so hate you.
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
A man that bears false witness against his neighbour is a maul, and a sword, and a sharp arrow.
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
Confidence in an unfaithful man in time of trouble is like a broken tooth, and a foot out of joint.
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
As he that takes away a garment in cold weather, and as vinegar upon alkali, so is he that sings songs to an heavy heart.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
If your enemy be hungry, give him bread to eat; and if he be thirsty, give him water to drink:
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
For you shall heap coals of fire upon his head, and the LORD shall reward you.
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
The north wind drives away rain: so does an angry countenance a backbiting tongue.
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
It is better to dwell in the corner of the housetop, than with a brawling woman and in a wide house.
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
As cold waters to a thirsty soul, so is good news from a far country.
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
A righteous man falling down before the wicked is as a troubled fountain, and a corrupt spring.
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
It is not good to eat much honey: so for men to search their own glory is not glory.
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
He that has no rule over his own spirit is like a city that is broken down, and without walls.