< Mithali 25 >
1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
THESE ARE ALSO PARABLES of Salomon, which the men of Hezekiah King of Iudah copied out.
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
The glorie of God is to conceale a thing secret: but the Kings honour is to search out a thing.
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
The heaues in height, and the earth in deepenes, and the Kings heart can no man search out.
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
Take the drosse from the siluer, and there shall proceede a vessell for the finer.
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
Take away the wicked from the King, and his throne shall be stablished in righteousnes.
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
Boast not thy selfe before the King, and stand not in the place of great men.
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
For it is better, that it be saide vnto thee, Come vp hither, then thou to be put lower in the presece of the prince whom thine eyes haue seene.
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
Goe not foorth hastily to strife, least thou know not what to doe in the ende thereof, when thy neighbour hath put thee to shame.
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
Debate thy matter with thy neighbour, and discouer not the secret to another,
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
Least he that heareth it put thee to shame, and thine infamie doe not cease.
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
A word spoken in his place, is like apples of golde with pictures of siluer.
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
He that reprooueth the wise, and the obedient eare, is as a golden earering and an ornament of fine golde.
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
As the colde of the snowe in the time of haruest, so is a faithfull messenger to them that send him: for he refresheth the soule of his masters.
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
A man that boasteth of false liberalitie, is like cloudes and winde without raine.
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
A Prince is pacified by staying of anger, and a soft tongue breaketh the bones.
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
If thou haue found hony, eate that is sufficient for thee, least thou be ouerfull, and vomit it.
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
Withdrawe thy foote from thy neighbours house, least he be weary of thee, and hate thee.
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
A man that beareth false witnes against his neighbour, is like an hammer and a sword, and a sharpe arrowe.
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
Confidence in an vnfaythfull man in time of trouble, is like a broken tooth and a sliding foote.
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
Hee that taketh away the garment in the colde season, is like vineger powred vpon nitre, or like him that singeth songs to an heauy heart.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
If hee that hateth thee be hungry, giue him bread to eate, and if he be thirstie, giue him water to drinke.
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
For thou shalt lay coles vpon his head, and the Lord shall recompense thee.
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
As the Northwinde driueth away the raine, so doeth an angry countenance the slandering tongue.
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
It is better to dwell in a corner of the house top, then with a contentious woman in a wide house.
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
As are the colde waters to a weary soule, so is good newes from a farre countery.
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
A righteous man falling downe before the wicked, is like a troubled well, and a corrupt spring.
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
It is not good to eate much hony: so to search their owne glory is not glory.
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
A man that refraineth not his appetite, is like a citie which is broken downe and without walles.