< Mithali 24 >

1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
NO tengas envidia de los hombres malos, ni desees estar con ellos:
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
Porque su corazón piensa en robar, é iniquidad hablan sus labios.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
Con sabiduría se edificará la casa, y con prudencia se afirmará:
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
Y con ciencia se henchirán las cámaras de todo bien preciado y agradable.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
El hombre sabio es fuerte; y de pujante vigor el hombre docto.
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
Porque con ingenio harás la guerra: y la salud está en la multitud de consejeros.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
Alta está para el insensato la sabiduría: en la puerta no abrirá él su boca.
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
Al que piensa mal hacer le llamarán hombre de malos pensamientos.
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
El pensamiento del necio es pecado: y abominación á los hombres el escarnecedor.
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
Si fueres flojo en el día de trabajo, tu fuerza será reducida.
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
Si dejares de librar los que son tomados para la muerte, y los que son llevados al degolladero;
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
Si dijeres: Ciertamente no lo supimos; ¿no lo entenderá el que pesa los corazones? El que mira por tu alma, él lo conocerá, y dará al hombre según sus obras.
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
Come, hijo mío, de la miel, porque es buena, y del panal dulce á tu paladar:
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
Tal será el conocimiento de la sabiduría á tu alma: si la hallares tendrá recompensa, y al fin tu esperanza no será cortada.
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
Oh impío, no aceches la tienda del justo, no saquees su cámara;
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
Porque siete veces cae el justo, y se torna á levantar; mas los impíos caerán en el mal.
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
Cuando cayere tu enemigo, no te huelgues; y cuando tropezare, no se alegre tu corazón:
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
Porque Jehová no lo mire, y le desagrade, y aparte de sobre él su enojo.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
No te entrometas con los malignos, ni tengas envidia de los impíos;
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
Porque para el malo no habrá [buen] fin, y la candela de los impíos será apagada.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
Teme á Jehová, hijo mío, y al rey; no te entrometas con los veleidosos:
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
Porque su quebrantamiento se levantará de repente; y el quebrantamiento de ambos, ¿quién lo comprende?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
También estas cosas [pertenecen] á los sabios. Tener respeto á personas en el juicio no es bueno.
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
El que dijere al malo, Justo eres, los pueblos lo maldecirán, y le detestarán las naciones:
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
Mas los que [lo] reprenden, serán agradables, y sobre ellos vendrá bendición de bien.
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
Besados serán los labios del que responde palabras rectas.
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
Apresta tu obra de afuera, y disponla en tu heredad; y después edificarás tu casa.
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
No seas sin causa testigo contra tu prójimo; y no lisonjees con tus labios.
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
No digas: Como me hizo, así le haré; daré el pago al hombre según su obra.
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
Pasé junto á la heredad del hombre perezoso, y junto á la viña del hombre falto de entendimiento;
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
Y he aquí que por toda ella habían ya crecido espinas, ortigas habían ya cubierto su haz, y su cerca de piedra estaba ya destruída.
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
Y yo miré, y púse[lo] en mi corazón: vi[lo], y tomé consejo.
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
Un poco de sueño, cabeceando otro poco, poniendo mano sobre mano otro poco para dormir;
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
Así vendrá como caminante tu necesidad, y tu pobreza como hombre de escudo.

< Mithali 24 >