< Mithali 24 >

1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
No tengas envidia de los hombres malos, ni el deseo de estar con ellos;
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
para que sus corazones traman la violencia y sus labios hablan de travesuras.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
A través de la sabiduría se construye una casa; mediante la comprensión se establece;
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
por conocimiento las habitaciones se llenan con todos los tesoros raros y hermosos.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
Un hombre sabio tiene un gran poder. Un hombre con conocimientos aumenta la fuerza,
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
pues con una sabia guía libras tu guerra, y la victoria está en muchos asesores.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
La sabiduría es demasiado elevada para un tonto. No abre la boca en la puerta.
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
El que conspira para hacer el mal se le llamará intrigante.
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
Los planes de la locura son pecado. El burlador es detestado por los hombres.
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
Si flaqueas en el momento de la dificultad, tu fuerza es pequeña.
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
¡Rescata a los que están siendo llevados a la muerte! En efecto, ¡retened a los que se tambalean hacia la matanza!
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
Si dices: “He aquí que no sabíamos esto” ¿acaso el que pesa los corazones no lo considera? El que guarda tu alma, ¿no lo sabe? ¿No ha de dar a cada uno según su trabajo?
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
Hijo mío, come miel, porque es buena, los excrementos del panal, que son dulces a su gusto;
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
así conocerás que la sabiduría es para tu alma. Si lo has encontrado, habrá una recompensa: Su esperanza no será cortada.
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
No aceches, malvado, contra la morada de los justos. No destruyas su lugar de descanso;
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
porque el justo cae siete veces y se levanta, pero los malvados son derribados por la calamidad.
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
No te alegres cuando tu enemigo caiga. No dejes que tu corazón se alegre cuando sea derrocado,
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
no sea que Yahvé lo vea y le desagrade, y aleja de él su ira.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
No te preocupes por los malhechores, ni tengas envidia de los malvados;
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
porque no habrá recompensa para el hombre malo. La lámpara de los malvados se apagará.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
Hijo mío, teme a Yahvé y al rey. No te unas a los rebeldes,
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
porque su calamidad surgirá de repente. ¿Quién sabe qué destrucción puede venir de ambos?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
Estos son también los dichos de los sabios: Mostrar parcialidad en el juicio no es bueno.
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
El que dice al impío: “Eres justo” los pueblos lo maldecirán, y las naciones lo aborrecerán —
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
pero les irá bien a los que condenen a los culpables, y una rica bendición vendrá sobre ellos.
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
Una respuesta sincera es como un beso en los labios.
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
Prepara tu trabajo en el exterior, y preparen sus campos. Después, construye tu casa.
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
No seas testigo contra tu prójimo sin motivo. No engañes con tus labios.
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
No digas: “Haré con él lo que él ha hecho conmigo”; Pagaré al hombre según su trabajo”.
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
Pasé por el campo del perezoso, por la viña del hombre vacío de entendimiento.
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
He aquí que todo estaba cubierto de espinas. Su superficie estaba cubierta de ortigas, y su muro de piedra fue derribado.
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
Entonces vi, y consideré bien. Vi y recibí instrucción:
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
un poco de sueño, un poco de sopor, un pequeño pliegue de las manos para dormir,
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
por lo que su pobreza vendrá como un ladrón y su necesidad como hombre armado.

< Mithali 24 >