< Mithali 24 >
1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
Não tenhas inveja dos homens malignos, nem desejes estar com eles,
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
Porque o seu coração medita a rapina, e os seus lábios falam a malícia.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
Com a sabedoria se edifica a casa, e com a inteligência se estabelece:
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
E pelo conhecimento se encherão as câmaras de todas as substâncias preciosas e deleitáveis.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
E o varão sábio é forte, e o varão de conhecimento consolida a força.
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
Porque com conselhos prudentes tu farás a guerra; e há vitória na multidão dos conselheiros.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
É demasiadamente alta para o tolo toda a sabedoria; na porta não abrirá a sua boca.
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
Aquele que cuida em fazer mal mestre de maus intentos o chamarão.
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
O pensamento do tolo é pecado, e é abominável aos homens o escarnecedor.
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
Se te mostrares frouxo no dia da angústia, a tua força será estreita.
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
Livra aos que estão tomados para a morte, e aos que levam para matança, se os poderes retirar.
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
Se disseres: Eis que o não sabemos: porventura aquele que pondera os corações não o entenderá? e aquele que atenta para a tua alma não o saberá? porque pagará ao homem conforme a sua obra.
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
Come mel, meu filho, porque é bom, e o favo de mel é doce ao teu paladar.
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
Tal será o conhecimento da sabedoria para a tua alma: se a achares, haverá para ti galardão, e não será cortada a tua expectação.
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
Não espies a habitação do justo, ó ímpio, nem assoles a sua câmara.
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
Porque sete vezes cairá o justo, e se levantará; mas os ímpios tropeçarão no mal
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
Quando cair o teu inimigo, não te alegres, nem quando tropeçar se regozije o teu coração.
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
Para que o Senhor o não veja, e seja mau aos seus olhos, e desvie dele a sua ira.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
Não te indignes acerca dos malfeitores, nem tenhas inveja dos ímpios,
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
Porque o maligno não terá galardão, e a lâmpada dos ímpios se apagará.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
Teme ao Senhor, filho meu, e ao rei, e não te entremetas com os que buscam mudança.
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
Porque de repente se levantará a sua perdição, e a ruína deles ambos quem a sabe?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
Também estes são provérbios dos sábios: Ter respeito a pessoas no juízo não é bom.
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
O que disser ao ímpio: Justo és: os povos o amaldiçoarão, as nações o detestarão.
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
Mas para os que o repreenderem haverá delícias, e sobre eles virá a benção do bem
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
Beijados serão os lábios do que responde com palavras retas.
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
Prepara de fora a tua obra, e aparelha-a no campo, e então edifica a tua casa.
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
Não sejas testemunha sem causa contra o teu próximo; porque enganarias com os teus beiços?
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
Não digas: Como ele me fez a mim, assim o farei eu a ele: pagarei a cada um segundo a sua obra.
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
Passei pelo campo do preguiçoso, e junto à vinha do homem falto de entendimento;
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
E eis que toda estava cheia de cardos, e a sua superfície coberta de ortigas, e a sua parede de pedra estava derribada.
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
O que tendo eu visto, o tomei no coração, e, vendo-o, recebi instrução.
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
Um pouco de sono, adormecendo um pouco; encruzando as mãos outro pouco, para estar deitado.
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
Assim te sobrevirá a tua pobreza como um caminhante, e a tua necessidade como um homem armado.