< Mithali 24 >
1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
Folge nicht bösen Leuten und wünsche nicht, bei ihnen zu sein.
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
Denn ihr Herz trachtet nach Schaden, und ihre Lippen raten zu Unglück.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
Durch Weisheit wird ein Haus gebauet und durch Verstand erhalten.
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
Durch ordentlich Haushalten werden die Kammern voll aller köstlichen, lieblichen Reichtümer.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
Ein weiser Mann ist stark und ein vernünftiger Mann ist mächtig von Kräften.
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
Denn mit Rat muß man Krieg führen; und wo viel Ratgeber sind, da ist der Sieg.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
Weisheit ist dem Narren zu hoch; er darf seinen Mund im Tor nicht auftun.
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
Wer ihm selbst Schaden tut, den heißt man billig einen Erzbösewicht.
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
Des Narren Tücke ist Sünde; und der Spötter ist ein Greuel vor den Leuten.
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
Der ist nicht stark, der in der Not nicht fest ist.
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
Errette die, so man töten will, und entzieh dich nicht von denen, die man würgen will.
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
Sprichst du: Siehe, wir verstehen's nicht; meinest du nicht, der die Herzen weiß, merket es, und der auf die Seele acht hat, kennet es und vergilt dem Menschen nach seinem Werk?
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
Iß, mein Sohn, Honig, denn es ist gut, und Honigseim ist süß in deinem Halse.
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
Also lerne die Weisheit für deine Seele. Wenn du sie findest, so wird's hernach wohlgehen, und deine Hoffnung wird nicht umsonst sein.
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
Laure nicht, als ein Gottloser, auf das Haus des Gerechten; verstöre seine Ruhe nicht!
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
Denn ein Gerechter fällt siebenmal und stehet wieder auf; aber die Gottlosen versinken in Unglück.
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
Freue dich des Falles deines Feindes nicht, und dein Herz sei nicht froh über seinem Unglück;
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
es möchte der HERR sehen und ihm übel gefallen und seinen Zorn von ihm wenden.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
Erzürne dich nicht über den Bösen und eifre nicht über die Gottlosen;
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
denn der Böse hat nichts zu hoffen, und die Leuchte der Gottlosen wird verlöschen.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
Mein Kind, fürchte den HERRN und den König und menge dich nicht unter die Aufrührerischen!
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
Denn ihr Unfall wird plötzlich entstehen; und wer weiß, wann beider Unglück kommt?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
Dies kommt auch von den Weisen: Die Person ansehen im Gericht ist nicht gut.
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
Wer zum Gottlosen spricht: Du bist fromm, dem fluchen die Leute und hasset das Volk.
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
Welche aber strafen, die gefallen wohl, und kommt ein reicher Segen auf sie.
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
Eine richtige Antwort ist wie ein lieblicher Kuß.
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
Richte draußen dein Geschäft aus und arbeite deinen Acker; danach baue dein Haus.
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
Sei nicht Zeuge ohne Ursache wider deinen Nächsten und betrüge nicht mit deinem Munde!
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
Sprich nicht: Wie man mir tut, so will ich wieder tun und einem jeglichen sein Werk vergelten.
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
Ich ging vor dem Acker des Faulen und vor dem Weinberge des Narren,
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
und siehe, da waren eitel Nesseln drauf und stund voll Disteln, und die Mauer war eingefallen.
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
Da ich das sah, nahm ich's zu Herzen und schauete und lernete dran.
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
Du willst ein wenig schlafen und ein wenig schlummern und ein wenig die Hände zusammentun, daß du ruhest;
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
aber es wird dir deine Armut kommen wie ein Wanderer und dein Mangel wie ein gewappneter Mann.