< Mithali 24 >

1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
Ne jalouse pas les hommes d’iniquité; ne souhaite pas de frayer avec eux;
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
car leur cœur machine des ruines, et leurs lèvres débitent l’injustice.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
C’Est par la sagesse que s’édifie la maison c’est par la raison qu’elle se consolide.
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
Grâce à l’intelligence, le logis se remplit de toute sorte de biens rares et précieux.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
Le sage est armé d’énergie, et l’homme d’expérience voit doubler sa force.
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
C’Est en suivant un plan habile que tu dois entreprendre la guerre; la victoire est assurée par la multitude des conseillers.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
Les données de la sagesse sont inaccessibles au sot; à la Porte, il n’ouvre pas la bouche.
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
Qui médite de faire le mal, on l’appelle l’homme aux noirs projets.
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
Le péché est une conception de la folie, et les gens ont horreur du persifleur.
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
Il faiblit au jour de la détresse: c’est que ton courage a l’haleine courte.
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
Sauve ceux qu’on traîne à la mort, ne manque pas de défendre ceux qui vont au supplice.
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
Tu diras peut-être: "Cet homme là, nous ne le connaissons pas!" Mais celui qui pénètre au. fond des cœurs comprend; celui qui veille sur ta vie sait, et il rétribue chacun selon ses œuvres.
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
Mange du miel, mon fils, car c’est bon; les rayons en seront doux à ton palais.
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
Telle est, sache-le bien, la sagesse pour ton âme; si tu t’en rends maître, il y a de l’avenir pour toi, ton espoir ne sera pas anéanti.
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
Méchant, pas de machination secrète contre la demeure du juste! Pas d’entreprises contre le lieu de sa résidence!
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
Car le juste tombe sept fois, et se relève; mais les méchants sont culbutés par le malheur.
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
Lorsque ton ennemi tombe, ne te réjouis point; s’il succombe, que ton cœur ne jubile pas!
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
L’Eternel verrait cela de mauvais œil, et il détournerait de lui sa colère.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
Ne porte pas envie aux malfaiteurs, ne jalouse pas les méchants;
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
car le méchant n’a pas d’avenir: la lumière des impies est fumeuse.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
Crains l’Eternel, mon fils, ainsi que le roi: ne te mêle pas aux novateurs;
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
car soudain, le désastre fond sur eux: qui peut mesurer les coups que leur réservent l’un et l’autre?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
Les sentences suivantes émanent également des sages: Faire acception de personnes en justice n’est pas une bonne chose.
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
Celui qui prononce sur le coupable en disant: "Tu es acquitté!" les peuples le maudissent, les gens l’exècrent.
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
Mais on est bienveillant pour ceux qui le répriment, et il leur vient des souhaits de bonheur.
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
C’Est comme un baiser des lèvres que de répliquer par dés paroles équitables.
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
Prépare-toi une occupation au dehors, déploie ton activité dans ton champ, puis, tu édifieras ta maison.
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
Ne témoigne pas sans motif contre ton prochain: prétendrais-tu exercer une séduction par tes lèvres?
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
Ne dis pas: "Comme il m’a traité, je le traiterai; je rends à chacun selon ses œuvres."
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
J’Ai passé près du champ d’un paresseux, près du vignoble d’un homme privé de sens.
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
Et voilà qu’il était tout envahi par l’ivraie; les ronces en recouvraient la surface, l’enclos de pierres était en ruines.
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
Je contemplai ce spectacle, j’y donnai mon attention, et de cette vue je tirai une leçon:
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
"Ah! dormir encore un peu, rester un peu assoupi, entrelacer un peu les mains pour reposer!"
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
"Cependant, la pauvreté s’introduit chez toi comme un rôdeur, et la misère comme un guerrier armé!"

< Mithali 24 >