< Mithali 24 >

1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
Sue thou not yuele men, desire thou not to be with hem.
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
For the soule of hem bithenkith raueyns, and her lippis speken fraudis.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
An hous schal be bildid bi wisdom, and schal be maad strong bi prudence.
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
Celeris schulen be fillid in teching, al riches preciouse and ful fair.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
A wijs man is strong, and a lerned man is stalworth and miyti.
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
For whi batel is bigunnun with ordenaunce, and helthe schal be, where many counsels ben.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
Wisdom is hiy to a fool; in the yate he schal not opene his mouth.
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
He that thenkith to do yuels, schal be clepid a fool.
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
The thouyte of a fool is synne; and a bacbitere is abhomynacioun of men.
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
If thou that hast slide, dispeirist in the dai of angwisch, thi strengthe schal be maad lesse.
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
Delyuere thou hem, that ben led to deth; and ceesse thou not to delyuere hem, that ben drawun to deth.
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
If thou seist, Strengthis suffisen not; he that is biholdere of the herte, vndirstondith, and no thing disseyueth the kepere of thi soule, and he schal yelde to a man bi hise werkis.
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
Mi sone, ete thou hony, for it is good; and an honycomb ful swete to thi throte.
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
`So and the techyng of wisdom is good to thi soule; and whanne thou hast founde it, thou schalt haue hope in the laste thingis, and thin hope schal not perische.
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
Aspie thou not, and seke not wickidnesse in the hous of a iust man, nether waste thou his reste.
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
For a iust man schal falle seuene sithis in the dai, and schal rise ayen; but wickid men schulen falle in to yuele.
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
Whanne thin enemye fallith, haue thou not ioye; and thin herte haue not ful out ioiyng in his fal;
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
lest perauenture the Lord se, and it displese hym, and he take awei his ire fro hym.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
Stryue thou not with `the worste men, nether sue thou wickid men.
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
For whi yuele men han not hope of thingis to comynge, and the lanterne of wickid men schal be quenchid.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
My sone, drede thou God, and the kyng; and be thou not medlid with bacbiteris.
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
For her perdicioun schal rise togidere sudenli, and who knowith the fal of euer either?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
Also these thingis that suen ben to wise men. It is not good to knowe a persoone in doom.
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
Puplis schulen curse hem, that seien to a wickid man, Thou art iust; and lynagis schulen holde hem abhomynable.
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
Thei that repreuen iustli synners, schulen be preisid; and blessing schal come on hem.
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
He that answerith riytful wordis, schal kisse lippis.
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
Make redi thi werk with outforth, and worche thi feelde dilygentli, that thou bilde thin hous aftirward.
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
Be thou not a witnesse with out resonable cause ayens thi neiybore; nether flatere thou ony man with thi lippis.
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
Seie thou not, As he dide to me, so Y schal do to him, and Y schal yelde to ech man aftir his werk.
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
I passide bi the feeld of a slow man, and bi the vyner of a fonned man; and, lo!
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
nettlis hadden fillid al, thornes hadden hilid the hiyere part therof, and the wal of stoonys with out morter was distried.
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
And whanne Y hadde seyn this thing, Y settide in myn herte, and bi ensaumple Y lernyde techyng.
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
Hou longe slepist thou, slow man? whanne schalt thou ryse fro sleep? Sotheli thou schalt slepe a litil, thou schalt nappe a litil, thou schalt ioyne togidere the hondis a litil, to take reste;
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
and thi nedynesse as a currour schal come to thee, and thi beggerie as an armed man.

< Mithali 24 >