< Mithali 24 >
1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
Ne zavidi opakim ljudima niti želi da budeš s njima.
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
Jer im srce smišlja nasilje i usne govore o nedjelu.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
Mudrošću se zida kuća i razborom utvrđuje,
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
i po znanju se pune klijeti svakim blagom dragocjenim i ljupkim.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
Bolji je mudar od jakoga i čovjek razuman od silne ljudine.
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
Jer s promišljanjem se ide u boj i pobjeda je u mnoštvu savjetnika.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
Previsoka je bezumnomu mudrost: zato na sudu ne otvara usta svojih!
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
Tko smišlja zlo zove se učitelj podmukli.
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
Ludost samo grijeh snuje, i podrugljivac je mrzak ljudima.
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
Kloneš li u dan bijede, bijedna je tvoja snaga.
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
Izbavi one koje vode u smrt; i spasavaj one koji posrćući idu na stratište.
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
Ako kažeš: “Nismo za to znali”, ne razumije li onaj koji ispituje srca? I ne znade li onaj koji ti čuva dušu? I ne plaća li on svakomu po njegovim djelima?
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
Jedi med, sine moj, jer je dobar, i saće je slatko nepcu tvome.
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
Takva je, znaj, i mudrost tvojoj duši: ako je nađeš, našao si budućnost i nada tvoja neće propasti.
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
Ne postavljaj, opaki, zasjede stanu pravednikovu, ne čini nasilja boravištu njegovu;
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
jer padne li pravednik i sedam puta, on ustaje, a opaki propadaju u nesreći.
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
Ne veseli se kad padne neprijatelj tvoj i ne kliči srcem kada on posrće,
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
da ne bi vidio Jahve i za zlo uzeo i obratio srdžbu svoju od njega.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
Nemoj se srditi zbog zločinaca, nemoj zavidjeti opakima,
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
jer zao čovjek nema budućnosti, svjetiljka opakih gasi se.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
Boj se Jahve, sine moj, i kralja: i ne buni se ni protiv jednoga ni protiv drugoga.
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
Jer iznenada provaljuje nesreća njihova i tko zna kad će doći propast njihova.
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
I ovo je od mudraca: Ne valja biti pristran na sudu.
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
Tko opakomu veli: “Pravedan si”, proklinju ga narodi i kunu puci;
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
a oni koji ga ukore nalaze zadovoljstvo, i na njih dolazi blagoslov sreće.
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
U usta ljubi tko odgovara pošteno.
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
Svrši svoj posao vani i uredi svoje polje, potom i kuću svoju zidaj.
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
Ne svjedoči lažno na bližnjega svoga: zar ćeš varati usnama svojim?
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
Ne reci: “Kako je on meni učinio, tako ću i ja njemu; platit ću tom čovjeku po djelu njegovu!”
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
Prolazio sam mimo polje nekog lijenčine i mimo vinograd nekog luđaka,
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
i gle, sve bijaše zaraslo u koprive, i sve pokrio čkalj, i kamena ograda porušena.
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
Vidjeh to i pohranih u srcu, promotrih i uzeh pouku:
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
“Još malo odspavaj, još malo odrijemaj, još malo podvij ruke za počinak,
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
i doći će tvoje siromaštvo kao skitač i oskudica kao oružanik!”