< Mithali 24 >
1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
你不要嫉妒恶人, 也不要起意与他们相处;
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
因为,他们的心图谋强暴, 他们的口谈论奸恶。
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
房屋因智慧建造, 又因聪明立稳;
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
其中因知识充满各样美好宝贵的财物。
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
智慧人大有能力; 有知识的人力上加力。
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
你去打仗,要凭智谋; 谋士众多,人便得胜。
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
智慧极高,非愚昧人所能及, 所以在城门内不敢开口。
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
设计作恶的, 必称为奸人。
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
愚妄人的思念乃是罪恶; 亵慢者为人所憎恶。
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
你在患难之日若胆怯, 你的力量就微小。
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
人被拉到死地,你要解救; 人将被杀,你须拦阻。
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
你若说:这事我未曾知道, 那衡量人心的岂不明白吗? 保守你命的岂不知道吗? 他岂不按各人所行的报应各人吗?
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
我儿,你要吃蜜,因为是好的; 吃蜂房下滴的蜜便觉甘甜。
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
你心得了智慧,也必觉得如此。 你若找着,至终必有善报; 你的指望也不致断绝。
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
你这恶人,不要埋伏攻击义人的家; 不要毁坏他安居之所。
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
因为,义人虽七次跌倒,仍必兴起; 恶人却被祸患倾倒。
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
你仇敌跌倒,你不要欢喜; 他倾倒,你心不要快乐;
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
恐怕耶和华看见就不喜悦, 将怒气从仇敌身上转过来。
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
不要为作恶的心怀不平, 也不要嫉妒恶人;
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
因为,恶人终不得善报; 恶人的灯也必熄灭。
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
我儿,你要敬畏耶和华与君王, 不要与反复无常的人结交,
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
因为他们的灾难必忽然而起。 耶和华与君王所施行的毁灭, 谁能知道呢?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
以下也是智慧人的箴言: 审判时看人情面是不好的。
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
对恶人说“你是义人”的, 这人万民必咒诅,列邦必憎恶。
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
责备恶人的,必得喜悦; 美好的福也必临到他。
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
应对正直的,犹如与人亲嘴。
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
你要在外头预备工料, 在田间办理整齐, 然后建造房屋。
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
不可无故作见证陷害邻舍, 也不可用嘴欺骗人。
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
不可说:人怎样待我,我也怎样待他; 我必照他所行的报复他。
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
我经过懒惰人的田地、 无知人的葡萄园,
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
荆棘长满了地皮, 刺草遮盖了田面, 石墙也坍塌了。
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
我看见就留心思想; 我看着就领了训诲。
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
再睡片时,打盹片时, 抱着手躺卧片时,
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
你的贫穷就必如强盗速来, 你的缺乏仿佛拿兵器的人来到。