< Mithali 24 >
1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
你不要妒忌作惡的人,不要希求與他們共處;
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
因為他們的心靈,只圖謀不軌;他們的嘴唇,只講論是非。
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
因著智慧,家庭得以興建;因著明智,家庭得以穩定。
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
各種珍奇可愛的寶物,因著智識可儲藏滿室。
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
智慧人勝於壯士,明智人強於勇士;
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
因為作戰須有智謀,勝利在於謀士眾多。
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
為愚昧的人,智慧太高妙;他在城門口,只好不開口。
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
籌劃作惡的人,可稱為陰險家。
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
愚人的計謀只是罪惡;狂妄的人為人所憎惡。
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
你若萎靡不振,到災難的日子,必然氣竭力盡。
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
被帶去受死的人,你應拯救他;行將被殺戮的人,你要挽救他。
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
或許你要說:「看! 我全不知道! 」難道那權衡人心的能不明瞭﹖難道監察你心靈的能不知道﹖他必按每人的作為還報每人。
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
我兒,你要吃蜜,因為蜜好;蜂房的蜜,香甜可口。
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
對你的靈魂,智慧也是這樣:你找得了她,必有好前途;你所希望的,決不會落空。
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
惡惡人對義人的家,不要圖謀不軌;對他的住所,不要加以破壞;
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
因為義人雖七次跌倒,仍然要起來;但是惡人一失足,必陷禍患中。
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
你的仇人跌倒,且不要高興;他若失足摔倒,且不要心喜;
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
免得上主看見而不快,因而撤消對他的忿怒。
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
對作惡的人,你不要動怒;對乖戾之徒,也不必嫉妒;
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
因為惡人終沒有好前途,惡人的燈必要熄滅。
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
我兒,上主和君王,你都要敬畏;對他們二者,皆不可觸怒;
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
因為他們的懲罰可突然而至;他們的摧殘,有誰能知曉﹖
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
以下是智者的箴言:在判案時,顧及情面,決不公平。
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
誰對惡人說:「你是正義的。」人民必罵他,百姓必恨他。
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
按公道加罰的,必事事順遂;美好的祝福,必臨於其身。
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
應答適宜的人,宛如與人接吻。
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
你要先在外經營好事業,在田間將工作準備停當,然後纔可建立你的家室。
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
不要輕易作證,反對你的近人;也不要以你的口舌,欺騙他人。
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
不可說:「人怎樣待我,我怎樣待人;照人之所行,我向他還報。」
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
我走過懶惰人的田地,經過愚昧人的葡萄園:
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
看,到處是荊棘,滿地是蒺黎,石牆也倒了!
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
我看了,便心下自思;我見了,取得了教訓:「
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
再睡片刻,再假寐片刻,再抱臂躺臥片刻」──
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
這樣,貧窮就要如同竊賊,困乏也要如同武士,向你侵襲。