< Mithali 23 >

1 Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
Wenn du sitzest, um mit einem regierenden Herrn zu speisen, merke wohl, wen du vor dir hast,
2 na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
und setze dir ein Messer an die Kehle, wenn du ein Gieriger bist.
3 Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
hege kein Gelüsten nach seinen Leckerbissen, denn es ist betrügliche Speise.
4 Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
Mühe dich nicht ab, reich zu werden, und von deiner darauf gerichteten Klugheit sage dich los.
5 Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
Sollen deine Augen auf den Reichtum losfliegen, er aber verschwunden sein? Denn gewißlich verschafft er sich Flügel, wie ein Adler, der gen Himmel fliegt.
6 Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
Sei nicht Tischgast des Mißgünstigen und hege kein Gelüsten nach seinen Leckerbissen.
7 maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
Denn wie einer, der für sich nachrechnet, so ist er; iß und trink! spricht er zu dir, aber sein Herz ist nicht bei dir.
8 Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
Den Bissen, den du gegessen hast, muß du wieder ausspeien und deine freundlichen Worte hast du umsonst verschwendet.
9 Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
Vor des Thörichten Ohren rede nicht, denn er hat nur Verachtung für den klugen Sinn deiner Worte.
10 Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
Verrücke nicht die Grenze der Witwe, und mache keinen Eingriff in der Verwaisten Äcker.
11 maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
Denn ihr Erlöser ist stark - der wird ihre Sache wider dich führen.
12 Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
Bringe her zur Zucht dein Herz und dein Ohren zu einsichtigen Reden.
13 Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
Entziehe dem Knaben nicht die Zucht; wenn du ihn mit der Rute schlägst, so stirbt er nicht davon.
14 Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol h7585)
Du zwar schlägst ihn mit der Rute, aber sein Leben errettest du von der Unterwelt. (Sheol h7585)
15 Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
Mein Sohn, wenn dein Herz weise wird, bin auch nicht in meinem Herzen fröhlich,
16 sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
und mein Innerstes frohlockt, wenn deine Lippen reden, was recht ist.
17 Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
Dein Herz ereifere sich nicht um der Sünder willen, sondern um der Furcht Jahwes willen allezeit.
18 Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
Wahrlich, es giebt noch eine Zukunft, und deine Hoffnung wird nicht zu nichte werden.
19 Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
Höre du, mein Sohn, und werde weise und laß dein Herz den geraden Weg gehen.
20 Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
Sei nicht unter den Weinsäufern, unter denen, die sich mit Fleischverprassen gütlich thun.
21 maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
Denn der Säufer und Prasser verarmt, und schläfriges Wesen giebt Lumpen zur Kleidung.
22 Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
Gehorche deinem Vater, der dich gezeugt hat, und verachte nicht, wenn sie alt geworden, deine Mutter.
23 Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
Wahrheit erwirb und verkaufe sie nicht, Weisheit und Zucht und Einsicht.
24 Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
Laut frohlockt eines Frommen Vater; und wer einen Weisen gezeugt hat, der freut sich über ihn.
25 Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
Es möge sich dein Vater und deine Mutter freuen, und möge frohlocken, die dich gebar.
26 Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
Gieb mir, mein Sohn, dein Herz und laß deinen Augen meine Wege wohlgefallen.
27 Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
Denn eine tiefe Grube ist die Hure und ein enger Brunnen die Auswärtige.
28 Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
Dazu liegt sie wie ein Räuber auf der Lauer und vermehrt die Treulosen unter den Menschen.
29 Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
Wer hat Ach? wer hat Wehe? wer Gezänk? wer Klage? wer Wunden ohne Ursache? wer hat trübe Augen?
30 Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
Die, welche bis spät beim Weine sitzen, die da kommen, um den Mischtrank zu prüfen.
31 Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
Sieh nicht nach dem Weine, wie er rötlich schillert, wie er im Becher so schön sich spiegelt, leicht hinuntergleitet.
32 Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
Hintennach beißt er wie eine Schlange und spritzt Gift wie ein Basilisk.
33 Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
Deine Augen werden Seltsames sehen, und dein Herz wird verkehrte Dinge reden.
34 Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
Und du wirst sein wie einer, der mitten im Meere liegt, ja wie einer, der oben auf dem Mastbaume liegt.
35 Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”
“Sie haben mich geschlagen, es that mir nichts wehe; sie haben mich geprügelt, ich spüre nichts; Wann werde ich aufwachen? aufs neue will ich mich ihm wieder ergeben!”

< Mithali 23 >