< Mithali 23 >

1 Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
Wenn du dich hinsetzest, um mit einem Herrscher zu speisen, so beachte wohl, wen du vor dir hast;
2 na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
und setze ein Messer an deine Kehle, wenn du gierig bist.
3 Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
Laß dich nicht gelüsten nach seinen Leckerbissen, denn sie sind eine trügliche Speise.
4 Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
Bemühe dich nicht, reich zu werden, laß ab von deiner Klugheit.
5 Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
Willst du deine Augen darauf hinfliegen lassen, und siehe, fort ist es? Denn sicherlich schafft es sich Flügel gleich dem Adler, der gen Himmel fliegt.
6 Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
Iß nicht das Brot des Scheelsehenden, und laß dich nicht gelüsten nach seinen Leckerbissen.
7 maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
Denn wie er es [O. wie einer, der es usw.] abmißt in seiner Seele, so ist er. "Iß und trink!", spricht er zu dir, aber sein Herz ist nicht mit dir.
8 Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
Deinen Bissen, den du gegessen hast, mußt du ausspeien, und deine freundlichen Worte wirst du verlieren.
9 Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
Rede nicht zu den Ohren eines Toren, denn er wird die Einsicht deiner Worte verachten.
10 Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
Verrücke nicht die alte Grenze, und dringe nicht ein in die Felder der Waisen.
11 maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
Denn ihr Erlöser ist stark; er wird ihren Rechtsstreit wider dich führen.
12 Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
Bringe dein Herz her zur Unterweisung, und deine Ohren zu den Worten der Erkenntnis.
13 Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
Entziehe dem Knaben nicht die Züchtigung; wenn du ihn mit der Rute schlägst, wird er nicht sterben.
14 Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol h7585)
Du schlägst ihn mit der Rute, und du errettest seine Seele von dem Scheol. (Sheol h7585)
15 Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
Mein Sohn, wenn dein Herz weise ist, so wird auch mein Herz sich freuen;
16 sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
und meine Nieren werden frohlocken, wenn deine Lippen Geradheit reden.
17 Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
Dein Herz beneide nicht die Sünder, sondern beeifere sich jeden Tag um die Furcht Jehovas.
18 Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
Wahrlich, es gibt ein Ende, [O. eine Zukunft] und deine Hoffnung wird nicht vernichtet werden.
19 Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
Höre du, mein Sohn, und werde weise, und leite dein Herz geradeaus auf dem Wege.
20 Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
Sei nicht unter Weinsäufern, noch unter denen, die Fleisch verprassen;
21 maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
denn ein Säufer und ein Schlemmer verarmen, und Schlummer kleidet in Lumpen.
22 Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
Höre auf deinen Vater, der dich gezeugt hat, und verachte deine Mutter nicht, wenn sie alt geworden ist.
23 Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
Kaufe Wahrheit und verkaufe sie nicht, Weisheit und Unterweisung und Verstand.
24 Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
Hoch frohlockt der Vater eines Gerechten; und wer einen Weisen gezeugt hat, der freut sich seiner.
25 Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
Freuen mögen sich dein Vater und deine Mutter, und frohlocken, die dich geboren!
26 Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
Gib mir, mein Sohn, dein Herz, und laß deine Augen Gefallen haben an meinen Wegen!
27 Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
Denn die Hure ist eine tiefe Grube und die Fremde [Eig. die Ausländerin] ein enger Brunnen;
28 Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
ja, sie lauert auf wie ein Räuber, und sie mehrt die Treulosen unter den Menschen.
29 Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
Wer hat Ach, wer hat Weh, wer Zänkereien, wer Klage, wer Wunden ohne Ursache? wer Trübung der Augen?
30 Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
Die spät beim Weine sitzen, die einkehren, um Mischtrank zu kosten.
31 Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
Sieh den Wein nicht an, wenn er sich rot zeigt, wenn er im Becher blinkt, leicht hinuntergleitet.
32 Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
Sein Ende ist, daß er beißt wie eine Schlange und sticht wie ein Basilisk.
33 Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
Deine Augen werden Seltsames sehen, [And. üb.: nach fremden Weibern blicken] und dein Herz wird verkehrte Dinge reden.
34 Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
Und du wirst sein wie einer, der im Herzen des Meeres liegt, und wie einer, der da liegt auf der Spitze eines Mastes.
35 Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”
"Man hat mich geschlagen, es schmerzte mich nicht; man hat mich geprügelt, ich fühlte es nicht. Wann werde ich aufwachen? Ich will es wieder tun, will ihn abermals aufsuchen."

< Mithali 23 >