< Mithali 23 >

1 Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
Quand tu seras assis pour manger avec le prince, considère attentivement ce qui est servi devant toi;
2 na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
Mets un couteau à ta gorge, si cependant tu es maître de ton âme.
3 Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
Ne désire pas des aliments de celui chez qui est un pain de mensonge.
4 Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
Ne travaille pas à t’enrichir; mais à ta prudence mets des bornes.
5 Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
Ne lève pas tes yeux vers des richesses que tu ne peux avoir; parce qu’elles se feront des ailes comme celles d’un aigle, et s’envoleront au ciel.
6 Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
Ne mange pas avec un homme envieux, et ne désire pas de ses mets;
7 maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
Parce que, semblable à un devin et à un augure, il juge de ce qu’il ignore. Mange et bois, te dira-t-il, et son cœur n’est pas avec toi.
8 Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
Les aliments que tu avais mangés, tu les rejetteras; et tu perdras tes sages discours.
9 Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
Ne parle pas à l’oreille des insensés, parce qu’ils mépriseront la doctrine que tu leur auras enseignée par tes paroles.
10 Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
Ne touche pas aux bornes des petits; et n’entre pas dans le champ des orphelins;
11 maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
Car leur proche est puissant; et lui-même jugera contre toi leur cause.
12 Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
Que ton cœur s’avance vers la doctrine, et tes oreilles vers les paroles de la science.
13 Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
Ne soustrais pas à l’enfant la discipline; car si tu le frappes de la verge, il ne mourra pas.
14 Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol h7585)
Tu le frapperas donc de la verge; et de l’enfer tu délivreras son âme. (Sheol h7585)
15 Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
Mon fils, si ton esprit est sage, mon cœur se réjouira avec toi;
16 sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
Et mes reins exulteront, lorsque tes lèvres parleront droiture.
17 Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
Que ton cœur ne porte pas envie aux pécheurs; mais dans la crainte du Seigneur sois tout le jour;
18 Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
Parce que tu auras l’espérance à ton dernier moment, et que ton attente ne sera pas frustrée.
19 Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
Ecoute, mon fils, et sois sage; et dirige ton esprit dans la bonne voie.
20 Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
Ne te trouve pas dans les festins des buveurs, ni dans les orgies de ceux qui apportent des viandes pour manger ensemble.
21 maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
Car ceux qui passent le temps à boire et qui payent leur écot, se ruineront, et l’assoupissement sera vêtu de haillons.
22 Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
Ecoute ton père qui t’a engendré; et ne méprise pas ta mère, lorsqu’elle aura vieilli.
23 Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
Achète la vérité, et ne vends pas la sagesse, la doctrine et l’intelligence.
24 Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
Le père du juste exulte; celui qui a engendré le sage se réjouira en lui.
25 Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
Que ton père et ta mère se réjouissent; et qu’elle exulte, celle qui t’a enfanté.
26 Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
Donne-moi ton cœur, mon fils; et que tes yeux gardent mes voies.
27 Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
Car c’est une fosse profonde, qu’une prostituée; et un puits étroit, qu’une étrangère.
28 Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
Elle dresse des embûches sur la voie comme un voleur; et ceux qu’elle verra n’être pas sur leurs gardes, elle les tuera.
29 Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
À qui malheur? au père de qui malheur? à qui les querelles? à qui les fosses? à qui les blessures sans motifs? à qui le trouble des yeux?
30 Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
N’est-ce pas à ceux qui s’arrêtent à boire le vin, et qui prennent goût à vider des coupes pleines?
31 Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
Ne regarde pas le vin, quand il jaunit, lorsque sa couleur brille dans le verre: il entre doucement;
32 Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
Mais à la fin, il mordra comme une couleuvre: et comme le basilic, il répandra son venin.
33 Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
Tes yeux verront les étrangères, et ton cœur dira des choses perverses.
34 Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
Et tu seras comme un homme dormant au milieu de la mer, et comme un pilote assoupi, le gouvernail ayant été perdu;
35 Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”
Et tu diras: Ils m’ont frappé, mais je n’en ai pas souffert; ils m’ont traîné, et moi je ne l’ai pas senti: quand me réveillerai-je, et trouverai-je encore du vin?

< Mithali 23 >