< Mithali 22 >
1 Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
El buen nombre es más deseable que las grandes riquezas, y el favor amoroso es mejor que la plata y el oro.
2 Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
Los ricos y los pobres tienen esto en común: Yahvé es el creador de todos ellos.
3 Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
Un hombre prudente ve el peligro y se esconde; pero los simples pasan, y sufren por ello.
4 Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
El resultado de la humildad y el temor a Yahvé es la riqueza, el honor y la vida.
5 Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
Espinas y trampas hay en el camino de los malvados; quien guarda su alma se aleja de ellos.
6 Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
Educa al niño en el camino que debe seguir, y cuando sea viejo no se apartará de él.
7 Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
Los ricos dominan a los pobres. El prestatario está al servicio del prestamista.
8 Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
El que siembra maldad cosecha problemas, y la vara de su furia será destruida.
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
El que tiene un ojo generoso será bendecido, porque comparte su comida con los pobres.
10 Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
Expulsa al burlón, y se acabará la contienda; sí, se acabarán las peleas y los insultos.
11 Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
El que ama la pureza de corazón y habla con gracia es el amigo del rey.
12 Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
Los ojos de Yahvé vigilan el conocimiento, pero frustra las palabras de los infieles.
13 Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
El perezoso dice: “¡Hay un león afuera! Me matarán en las calles”.
14 Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
La boca de una adúltera es un pozo profundo. El que está bajo la ira de Yahvé caerá en ella.
15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
La locura está ligada al corazón de un niño; la vara de la disciplina lo aleja de él.
16 Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
El que oprime al pobre para su propio aumento y el que da al rico, ambos llegan a la pobreza.
17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
Vuelve tu oído y escucha las palabras de los sabios. Aplica tu corazón a mis enseñanzas.
18 maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
Porque es una cosa agradable si las guardas dentro de ti, si todos ellos están listos en sus labios.
19 Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
Hoy te enseño, incluso a ti, para que tu confianza esté en Yahvé.
20 Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
¿No te he escrito treinta cosas excelentes de consejo y conocimiento,
21 kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
Para enseñarte la verdad, palabras fiables, para dar respuestas sólidas a los que te enviaron?
22 Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
No exploten al pobre porque es pobre; y no aplastar a los necesitados en los tribunales;
23 maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
porque Yahvé defenderá su caso, y saquean la vida de los que los saquean.
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
No te hagas amigo de un hombre de mal genio. No te asocies con quien alberga ira,
25 au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
para que no aprendas sus caminos y atrapar tu alma.
26 Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
No seas de los que golpean las manos, de los que son garantía de las deudas.
27 Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
Si no tienes medios para pagar, ¿por qué debería quitarte la cama de debajo de ti?
28 Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
No muevas el antiguo mojón que sus padres han establecido.
29 Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.
¿Has visto hombre diligente en su obra? Estará delante de los reyes y no de la gentuza.