< Mithali 22 >

1 Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
melius est nomen bonum quam divitiae multae super argentum et aurum gratia bona
2 Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
dives et pauper obviaverunt sibi utriusque operator est Dominus
3 Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
callidus vidit malum et abscondit se innocens pertransiit et adflictus est damno
4 Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
finis modestiae timor Domini divitiae et gloria et vita
5 Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
arma et gladii in via perversi custos animae suae longe recedit ab eis
6 Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
proverbium est adulescens iuxta viam suam etiam cum senuerit non recedet ab ea
7 Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
dives pauperibus imperat et qui accipit mutuum servus est fenerantis
8 Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
qui seminat iniquitatem metet mala et virga irae suae consummabitur
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
qui pronus est ad misericordiam benedicetur de panibus enim suis dedit pauperi
10 Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
eice derisorem et exibit cum eo iurgium cessabuntque causae et contumeliae
11 Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
qui diligit cordis munditiam propter gratiam labiorum suorum habebit amicum regem
12 Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
oculi Domini custodiunt scientiam et subplantantur verba iniqui
13 Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
dicit piger leo foris in medio platearum occidendus sum
14 Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
fovea profunda os alienae cui iratus est Dominus incidet in eam
15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
stultitia conligata est in corde pueri et virga disciplinae fugabit eam
16 Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
qui calumniatur pauperem ut augeat divitias suas dabit ipse ditiori et egebit
17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
inclina aurem tuam et audi verba sapientium adpone autem cor ad doctrinam meam
18 maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
quae pulchra erit tibi cum servaveris eam in ventre tuo et redundabit in labiis tuis
19 Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
ut sit in Domino fiducia tua unde et ostendi eam tibi hodie
20 Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
ecce descripsi eam tibi tripliciter in cogitationibus et scientia
21 kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
ut ostenderem tibi firmitatem et eloquia veritatis respondere ex his illi qui misit te
22 Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
non facias violentiam pauperi quia pauper est neque conteras egenum in porta
23 maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
quia Dominus iudicabit causam eius et configet eos qui confixerint animam eius
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
noli esse amicus homini iracundo neque ambules cum viro furioso
25 au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
ne forte discas semitas eius et sumas scandalum animae tuae
26 Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
noli esse cum his qui defigunt manus suas et qui vades se offerunt pro debitis
27 Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
si enim non habes unde restituas quid causae est ut tollat operimentum de cubili tuo
28 Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
ne transgrediaris terminos antiquos quos posuerunt patres tui
29 Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.
vidisti virum velocem in opere suo coram regibus stabit nec erit ante ignobiles

< Mithali 22 >