< Mithali 22 >

1 Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
Melius est nomen bonum, quam divitiae multae: super argentum et aurum, gratia bona.
2 Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
Dives, et pauper obviaverunt sibi: utriusque operator est Dominus.
3 Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
Callidus videt malum, et abscondit se: innocens pertransiit, et afflictus est damno.
4 Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
Finis modestiae timor Domini, divitiae et gloria et vita.
5 Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
Arma et gladii in via perversi: custos autem animae suae longe recedit ab eis.
6 Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
Proverbium est: Adolescens iuxta viam suam, etiam cum senuerit, non recedet ab ea.
7 Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
Dives pauperibus imperat: et qui accipit mutuum, servus est foenerantis.
8 Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
Qui seminat iniquitatem, metet mala, et virga irae suae consummabitur.
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
Qui pronus est ad misericordiam, benedicetur: de panibus enim suis dedit pauperi. Victoriam et honorem acquiret qui dat munera: animam autem aufert accipientium.
10 Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
Eiice derisorem, et exibit cum eo iurgium, cessabuntque causae et contumeliae.
11 Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
Qui diligit cordis munditiam, propter gratiam labiorum suorum habebit amicum regem.
12 Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
Oculi Domini custodiunt scientiam: et supplantantur verba iniqui.
13 Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
Dicit piger: Leo est foris, in medio platearum occidendus sum.
14 Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
Fovea profunda, os alienae: cui iratus est Dominus, incidet in eam.
15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
Stultitia colligata est in corde pueri, et virga disciplinae fugabit eam.
16 Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
Qui calumniatur pauperem, ut augeat divitias suas, dabit ipse ditiori, et egebit.
17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
Fili mi! Inclina aurem tuam, et audi verba sapientium: appone autem cor ad doctrinam meam.
18 maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
quae pulchra erit tibi, cum servaveris eam in ventre tuo, et redundabit in labiis tuis:
19 Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
Ut sit in Domino fiducia tua, unde et ostendi eam tibi hodie.
20 Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
Ecce descripsi eam tibi tripliciter, in cogitationibus et scientia:
21 kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
ut ostenderem tibi firmitatem, et eloquia veritatis, respondere ex his illis, qui miserunt te.
22 Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
Non facias violentiam pauperi, quia pauper est: neque conteras egenum in porta:
23 maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
quia iudicabit Dominus causam eius, et configet eos, qui confixerunt animam eius.
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
Noli esse amicus homini iracundo, neque ambules cum viro furioso:
25 au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
ne forte discas semitas eius, et sumas scandalum animae tuae.
26 Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
Noli esse cum his, qui defigunt manus suas, et qui vades se offerunt pro debitis:
27 Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
si enim non habes unde restituas, quid causae est ut tollat operimentum de cubili tuo?
28 Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
Ne transgrediaris terminos antiquos, quos posuerunt patres tui.
29 Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.
Vidisti virum velocem in opere suo? coram regibus stabit, nec erit ante ignobiles.

< Mithali 22 >