< Mithali 22 >

1 Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
נבחר שם מעשר רב מכסף ומזהב חן טוב
2 Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
עשיר ורש נפגשו עשה כלם יהוה
3 Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
ערום ראה רעה ויסתר (ונסתר) ופתיים עברו ונענשו
4 Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
עקב ענוה יראת יהוה עשר וכבוד וחיים
5 Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
צנים פחים בדרך עקש שומר נפשו ירחק מהם
6 Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
חנך לנער על-פי דרכו-- גם כי-יזקין לא-יסור ממנה
7 Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
עשיר ברשים ימשול ועבד לוה לאיש מלוה
8 Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
זורע עולה יקצור- (יקצר-) און ושבט עברתו יכלה
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
טוב-עין הוא יברך כי-נתן מלחמו לדל
10 Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
גרש לץ ויצא מדון וישבת דין וקלון
11 Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
אהב טהור- (טהר-) לב-- חן שפתיו רעהו מלך
12 Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
עיני יהוה נצרו דעת ויסלף דברי בגד
13 Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
אמר עצל ארי בחוץ בתוך רחבות ארצח
14 Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
שוחה עמקה פי זרות זעום יהוה יפול- (יפל-) שם
15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
אולת קשורה בלב-נער שבט מוסר ירחיקנה ממנו
16 Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
עשק דל להרבות לו-- נתן לעשיר אך-למחסור
17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
הט אזנך--ושמע דברי חכמים ולבך תשית לדעתי
18 maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
כי-נעים כי-תשמרם בבטנך יכנו יחדו על-שפתיך
19 Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
להיות ביהוה מבטחך-- הודעתיך היום אף-אתה
20 Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
הלא כתבתי לך שלשום (שלשים)-- במעצות ודעת
21 kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
להודיעך--קשט אמרי אמת להשיב אמרים אמת לשלחיך
22 Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
אל-תגזל-דל כי דל-הוא ואל-תדכא עני בשער
23 maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
כי-יהוה יריב ריבם וקבע את-קבעיהם נפש
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
אל-תתרע את-בעל אף ואת-איש חמות לא תבוא
25 au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
פן-תאלף ארחתו ולקחת מוקש לנפשך
26 Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
אל-תהי בתקעי-כף בערבים משאות
27 Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
אם-אין-לך לשלם-- למה יקח משכבך מתחתיך
28 Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
אל-תסג גבול עולם-- אשר עשו אבותיך
29 Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.
חזית איש מהיר במלאכתו-- לפני-מלכים יתיצב בל-יתיצב לפני חשכים

< Mithali 22 >