< Mithali 22 >
1 Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
Betere is a good name, than many richessis; for good grace is aboue siluer and gold.
2 Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
A riche man and a pore man metten hem silf; the Lord is worchere of euer eithir.
3 Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
A felle man seeth yuel, and hidith him silf; and an innocent man passid, and he was turmentid bi harm.
4 Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
The ende of temperaunce is the drede of the Lord; richessis, and glorye, and lijf.
5 Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
Armuris and swerdis ben in the weie of a weiward man; but the kepere of his soule goith awey fer fro tho.
6 Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
It is a prouerbe, A yong wexynge man bisidis his weie, and whanne he hath wexe elde, he schal not go awei fro it.
7 Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
A riche man comaundith to pore men; and he that takith borewyng, is the seruaunt of the leenere.
8 Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
He that sowith wickidnes, schal repe yuels; and the yerde of his yre schal be endid.
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
He that is redi to merci, schal be blessid; for of his looues he yaf to a pore man. He that yyueth yiftis, schal gete victorie and onour; forsothe he takith awei the soule of the takeris.
10 Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
Caste thou out a scornere, and strijf schal go out with hym; and causis and dispisyngis schulen ceesse.
11 Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
He that loueth the clennesse of herte, schal haue the kyng a freend, for the grace of hise lippis.
12 Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
The iyen of the Lord kepen kunnyng; and the wordis of a wickid man ben disseyued.
13 Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
A slow man schal seie, A lioun is withoutforth; Y schal be slayn in the myddis of the stretis.
14 Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
The mouth of an alien womman is a deep diche; he to whom the Lord is wrooth, schal falle in to it.
15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
Foli is boundun togidere in the herte of a child; and a yerde of chastisyng schal dryue it awey.
16 Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
He that falsli chalengith a pore man, to encreesse hise owne richessis, schal yyue to a richere man, and schal be nedi.
17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
My sone, bowe doun thin eere, and here thou the wordis of wise men; but sette thou the herte to my techyng.
18 maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
That schal be fair to thee, whanne thou hast kept it in thin herte, and it schal flowe ayen in thi lippis.
19 Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
That thi trist be in the Lord; wherfor and Y haue schewid it to thee to dai.
20 Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
Lo! Y haue discryued it in thre maneres, in thouytis and kunnyng,
21 kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
that Y schulde schewe to thee the sadnesse and spechis of trewthe; to answere of these thingis to hem, that senten thee.
22 Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
Do thou not violence to a pore man, for he is pore; nethir defoule thou a nedi man in the yate.
23 maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
For the Lord schal deme his cause, and he schal turmente hem, that turmentiden his soule.
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
Nyle thou be freend to a wrathful man, nether go thou with a wood man;
25 au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
lest perauenture thou lerne hise weies, and take sclaundir to thi soule.
26 Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
Nyle thou be with hem that oblischen her hondis, and that proferen hem silf borewis for dettis; for if he hath not wherof he schal restore,
27 Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
what of cause is, that thou take awei hilyng fro thi bed?
28 Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
Go thou not ouer the elde markis, whiche thi faders han set.
29 Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.
Thou hast seyn a man smert in his werk; he schal stonde bifore kyngis, and he schal not be bifor vnnoble men.