< Mithali 22 >

1 Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
美名勝過大財; 恩寵強如金銀。
2 Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
富戶窮人在世相遇, 都為耶和華所造。
3 Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
通達人見禍藏躲; 愚蒙人前往受害。
4 Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
敬畏耶和華心存謙卑, 就得富有、尊榮、生命為賞賜。
5 Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
乖僻人的路上有荊棘和網羅; 保守自己生命的,必要遠離。
6 Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
教養孩童,使他走當行的道, 就是到老他也不偏離。
7 Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
富戶管轄窮人; 欠債的是債主的僕人。
8 Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
撒罪孽的,必收災禍; 他逞怒的杖也必廢掉。
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
眼目慈善的,就必蒙福, 因他將食物分給窮人。
10 Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
趕出褻慢人,爭端就消除; 紛爭和羞辱也必止息。
11 Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
喜愛清心的人因他嘴上的恩言, 王必與他為友。
12 Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
耶和華的眼目眷顧聰明人, 卻傾敗奸詐人的言語。
13 Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
懶惰人說:外頭有獅子; 我在街上就必被殺。
14 Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
淫婦的口為深坑; 耶和華所憎惡的,必陷在其中。
15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
愚蒙迷住孩童的心, 用管教的杖可以遠遠趕除。
16 Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
欺壓貧窮為要利己的, 並送禮與富戶的,都必缺乏。
17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
你須側耳聽受智慧人的言語, 留心領會我的知識。
18 maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
你若心中存記, 嘴上咬定,這便為美。
19 Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
我今日以此特特指教你, 為要使你倚靠耶和華。
20 Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
謀略和知識的美事, 我豈沒有寫給你嗎?
21 kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
要使你知道真言的實理, 你好將真言回覆那打發你來的人。
22 Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
貧窮人,你不可因他貧窮就搶奪他的物, 也不可在城門口欺壓困苦人;
23 maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
因耶和華必為他辨屈; 搶奪他的,耶和華必奪取那人的命。
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
好生氣的人,不可與他結交; 暴怒的人,不可與他來往;
25 au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
恐怕你效法他的行為, 自己就陷在網羅裏。
26 Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
不要與人擊掌, 不要為欠債的作保。
27 Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
你若沒有甚麼償還, 何必使人奪去你睡臥的床呢?
28 Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
你先祖所立的地界, 你不可挪移。
29 Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.
你看見辦事殷勤的人嗎? 他必站在君王面前, 必不站在下賤人面前。

< Mithali 22 >