< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
Le cœur du roi est un courant d’eau dans la main de l’Éternel; Il l’incline partout où il veut.
2 Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
Toutes les voies de l’homme sont droites à ses yeux; Mais celui qui pèse les cœurs, c’est l’Éternel.
3 Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
La pratique de la justice et de l’équité, Voilà ce que l’Éternel préfère aux sacrifices.
4 Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
Des regards hautains et un cœur qui s’enfle, Cette lampe des méchants, ce n’est que péché.
5 Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
Les projets de l’homme diligent ne mènent qu’à l’abondance, Mais celui qui agit avec précipitation n’arrive qu’à la disette.
6 Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
Des trésors acquis par une langue mensongère Sont une vanité fugitive et l’avant-coureur de la mort.
7 Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
La violence des méchants les emporte, Parce qu’ils refusent de faire ce qui est juste.
8 Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
Le coupable suit des voies détournées, Mais l’innocent agit avec droiture.
9 Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
Mieux vaut habiter à l’angle d’un toit, Que de partager la demeure d’une femme querelleuse.
10 Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
L’âme du méchant désire le mal; Son ami ne trouve pas grâce à ses yeux.
11 Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
Quand on châtie le moqueur, le sot devient sage; Et quand on instruit le sage, il accueille la science.
12 Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
Le juste considère la maison du méchant; L’Éternel précipite les méchants dans le malheur.
13 Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
Celui qui ferme son oreille au cri du pauvre Criera lui-même et n’aura point de réponse.
14 Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
Un don fait en secret apaise la colère, Et un présent fait en cachette calme une fureur violente.
15 Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
C’est une joie pour le juste de pratiquer la justice, Mais la ruine est pour ceux qui font le mal.
16 Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
L’homme qui s’écarte du chemin de la sagesse Reposera dans l’assemblée des morts.
17 Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
Celui qui aime la joie reste dans l’indigence; Celui qui aime le vin et l’huile ne s’enrichit pas.
18 Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
Le méchant sert de rançon pour le juste, Et le perfide pour les hommes droits.
19 Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
Mieux vaut habiter dans une terre déserte, Qu’avec une femme querelleuse et irritable.
20 Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
De précieux trésors et de l’huile sont dans la demeure du sage; Mais l’homme insensé les engloutit.
21 Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
Celui qui poursuit la justice et la bonté Trouve la vie, la justice et la gloire.
22 Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
Le sage monte dans la ville des héros, Et il abat la force qui lui donnait de l’assurance.
23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
Celui qui veille sur sa bouche et sur sa langue Préserve son âme des angoisses.
24 Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
L’orgueilleux, le hautain, s’appelle un moqueur; Il agit avec la fureur de l’arrogance.
25 Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
Les désirs du paresseux le tuent, Parce que ses mains refusent de travailler;
26 Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
Tout le jour il éprouve des désirs; Mais le juste donne sans parcimonie.
27 Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
Le sacrifice des méchants est quelque chose d’abominable; Combien plus quand ils l’offrent avec des pensées criminelles!
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
Le témoin menteur périra, Mais l’homme qui écoute parlera toujours.
29 Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
Le méchant prend un air effronté, Mais l’homme droit affermit sa voie.
30 Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
Il n’y a ni sagesse, ni intelligence, Ni conseil, en face de l’Éternel.
31 Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.
Le cheval est équipé pour le jour de la bataille, Mais la délivrance appartient à l’Éternel.

< Mithali 21 >