< Mithali 21 >
1 Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
Tel est le cours de l'eau, tel est le cœur du roi dans la main de Dieu; de quelque côté qu'il veuille l'incliner, c'est là qu'Il le dirige.
2 Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
Tout homme semble juste à ses yeux; mais Dieu dirige les cœurs.
3 Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
Faire des choses justes et dire la vérité est plus agréable au Seigneur que le sang des victimes.
4 Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
Le cœur de l'audacieux est superbe dans son insolence; la lampe des impies est le péché.
5 Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6 Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
Amasser des trésors avec une langue trompeuse, c'est poursuivre des vanités sur les filets de la mort.
7 Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
La destruction habitera avec les impies, parce qu'ils ne veulent pas pratiquer la justice.
8 Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
Devant les hommes tortueux Dieu place des voies tortueuses; car Ses œuvres sont droites et pures.
9 Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
Mieux vaut demeurer dans un carrefour en plein air, que dans une grande maison bien crépie avec l'iniquité.
10 Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
Nul homme ne sera miséricordieux pour l'âme des impies.
11 Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
La punition de l'intempérant rend l'innocent plus réfléchi; l'homme sage et intelligent en reçoit une leçon.
12 Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
Le juste pénètre le cœur des impies, et les méprise à cause de leur malice.
13 Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
Celui qui ferme l'oreille au cri du faible criera lui-même, et nul ne l'écoutera.
14 Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
Un don secret détourne les colères; celui qui épargne les présents excite de violents courroux.
15 Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
La joie du juste est de faire justice; le saint n'est pas pur aux yeux des méchants.
16 Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
L'homme qui s'égare loin des voies de la justice se reposera dans l'assemblée des géants.
17 Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
L'indigent aime la joie; il désire le vin et l'huile en abondance.
18 Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
Les déréglés sont en abomination aux justes.
19 Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
Mieux vaut habiter le désert qu'avec une femme bavarde, colère et querelleuse.
20 Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
Un trésor désirable reposera sur la bouche du sage; mais les insensés le dévorent.
21 Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
Les voies de la justice et de la miséricorde conduisent à la vie et à la gloire.
22 Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
Le sage a pris d'assaut les villes fortes; il a démoli les forteresses sur lesquelles comptaient les impies.
23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
Celui qui est maître de sa bouche et de sa langue garde son âme de la tribulation.
24 Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
L'homme audacieux, arrogant et présomptueux peut être appelé un fléau; le vindicatif n'est pas dans la loi.
25 Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
Les désirs tuent le paresseux; car ses mains ne se lèvent pas pour faire quoi que ce soit.
26 Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
L'impie, durant tout le jour, a des désirs mauvais; le juste n'est avare ni de compassion ni de miséricorde.
27 Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
Les sacrifices des impies sont en abomination au Seigneur; car ils les offrent le cœur plein d'iniquité.
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
Le faux témoin périra; un homme docile parlera avec réserve.
29 Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
L'impie compose effrontément son visage; mais l'homme droit saura bien discerner ses voies.
30 Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
Il n'est point de sagesse, point de courage, point de raison chez l'impie.
31 Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.
Le cheval est tout prêt pour le jour du combat; mais le secours vient de Dieu.