< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
Yahweh controls what kings do [MTY] [like] he controls how streams flow; he causes kings to do just what he wants them to do.
2 Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
People always think that what they do is right, but Yahweh judges our (motives/reasons [for doing things)] [MTY].
3 Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
Doing what is right and fair is more acceptable to Yahweh than [bringing] sacrifices [to him].
4 Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
Being proud and arrogant [DOU] is [like] a lamp [MTY] [that guides] wicked people; being proud and arrogant characterizes (wicked people’s whole behavior/everything that wicked people do).
5 Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
People who plan carefully will surely have plenty [of what they need]; those who act too quickly [to become rich] will become poor.
6 Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
Money that people acquire [by cheating others] by lying [MTY] to them will soon disappear [like] a mist, and doing that will [soon] lead to their death.
7 Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
Wicked [people] refuse to do what is right/just, but they will be ruined because of the violent things [PRS] that they do.
8 Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
Guilty [people continually do what is evil; it is as though] [MET] they are walking on a crooked road; but righteous/innocent people [always] do what is right.
9 Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
It is better to live in the corner of an attic/housetop [by yourself] than to live inside the house with a wife who is always nagging.
10 Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
Wicked [people] [SYN] are always wanting [to do what is] evil; they never act mercifully toward anyone.
11 Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
When those who ridicule [others] are punished, [even] those who do not have good sense [see that, and] they become wise, and when those who are wise are taught, they become wiser.
12 Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
[God], the one [who is completely] righteous, knows [what happens inside] the houses of wicked [people], and [he will cause] those people to be completely ruined/destroyed.
13 Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
There are people who refuse to listen when poor people cry out [for help]; [but some day] they themselves will cry out [for help], and no one will hear them.
14 Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
When someone is angry [with you], if you secretly give him a gift, he will stop being angry.
15 Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
Good/Righteous [people] are happy when they [see others do] what is just/fair, but those who do what is evil are terrified [when they think about what may happen to them].
16 Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
Those who stop behaving like those who have good sense behave will [soon] discover that they have gone to the place where dead people are.
17 Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
Those who spend their money to buy (things that give them pleasure/things that cause them to feel happy) will become poor; those who love [to spend money to buy] wine and nice/fancy food [MTY] will never become rich.
18 Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
Wicked [people] bring on themselves the sufferings that they were trying to cause righteous [people] to experience [DOU].
19 Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
It is better to live [alone] in a desert than [to live] with a wife who is [always] nagging and complaining.
20 Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
Wise people have many valuable things in their houses, but foolish people [quickly] spend/waste [all their money].
21 Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
Those who [always] try to act in a fair and kind way [toward others] will live [a long time] and be honored/respected.
22 Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
A wise army commander [helps his troops] climb over a wall [to attack] a city that is defended by a strong army, with the result that they are able to (get over/destroy) the high walls that their enemies trusted [would protect them].
23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
Those who are very careful about what they say [MTY] are [able to] avoid trouble.
24 Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
Those who make fun of [everything that is good] are proud and conceited [DOU]; they [always] act in an inconsiderate way [toward others].
25 Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
Lazy people, who refuse to work, [will] die [of hunger] because they [SYN] do not earn [money to buy food].
26 Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
All during the day [wicked people] desire to obtain things, but righteous [people] have plenty, [with the result that] they [are able to] give things generously to others.
27 Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
[Yahweh] detests the sacrifices that wicked [people] offer [to him]; [but he] detests it even more when they [think that they will escape being punished for] their evil deeds because of the sacrifices that they bring.
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
Those who tell lies in court will be punished; no one stops/silences witnesses who say what is truthful/reliable.
29 Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
Wicked people pretend [that they know everything], but righteous people think carefully about [what will happen because of] what they do.
30 Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
[Thinking that we are] wise, and that we understand many things, and that we have good insight, does not help us if Yahweh is (acting against/not pleased with) us.
31 Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.
We [can] get horses ready to fight in a battle, but Yahweh is the one who enables us to (win victories/defeat our enemies).

< Mithali 21 >