< Mithali 21 >
1 Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
stream water heart king in/on/with hand LORD upon all which to delight in to stretch him
2 Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
all way: conduct man upright in/on/with eye his and to measure heart LORD
3 Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
to make: do righteousness and justice to choose to/for LORD from sacrifice
4 Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
height eye and broad: arrogant heart lamp wicked sin
5 Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
plot sharp surely to/for advantage and all to hasten surely to/for need
6 Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
work treasure in/on/with tongue deception vanity to drive to seek death
7 Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
violence wicked to drag/chew/saw them for to refuse to/for to make: do justice
8 Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
crooked way: conduct man guilty and pure upright work his
9 Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
pleasant to/for to dwell upon corner roof from woman: wife contention and house: home fellow
10 Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
soul wicked to desire bad: evil not be gracious in/on/with eye his neighbor his
11 Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
in/on/with to fine to mock be wise simple and in/on/with be prudent to/for wise to take: recieve knowledge
12 Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
be prudent righteous to/for house: household wicked to pervert wicked to/for bad: evil
13 Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
to shutter ear his from outcry poor also he/she/it to call: call out and not to answer
14 Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
gift in/on/with secrecy to subdue face: anger and bribe in/on/with bosom: secret rage strong
15 Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
joy to/for righteous to make: do justice and terror to/for to work evil: wickedness
16 Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
man to go astray from way: conduct be prudent in/on/with assembly shade to rest
17 Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
man need to love: lover joy to love: lover wine and oil not to enrich
18 Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
ransom to/for righteous wicked and underneath: instead upright to act treacherously
19 Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
pleasant to dwell in/on/with land: country/planet wilderness from woman (contention *Q(K)*) and vexation
20 Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
treasure to desire and oil in/on/with pasture wise and fool man to swallow up him
21 Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
to pursue righteousness and kindness to find life righteousness and glory
22 Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
city mighty man to ascend: rise wise and to go down strength confidence her
23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
to keep: guard lip his and tongue his to keep: guard from distress soul: myself his
24 Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
arrogant proud to mock name his to make: do in/on/with fury arrogance
25 Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
desire sluggish to die him for to refuse hand his to/for to make: do
26 Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
all [the] day to desire desire and righteous to give: give and not to withhold
27 Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
sacrifice wicked abomination also for in/on/with wickedness to come (in): bring him
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
witness lie to perish and man to hear: hear to/for perpetuity to speak: speak
29 Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
be strong man wicked in/on/with face his and upright he/she/it (to understand way: conduct his *Q(K)*)
30 Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
nothing wisdom and nothing understanding and nothing counsel to/for before LORD
31 Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.
horse to establish: prepare to/for day battle and to/for LORD [the] deliverance: victory