< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
The Kings heart is in the hand of the Lord, as the riuers of waters: he turneth it whithersoeuer it pleaseth him.
2 Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
Euery way of a man is right in his owne eyes: but the Lord pondereth the hearts.
3 Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
To doe iustice and iudgement is more acceptable to the Lord then sacrifice.
4 Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
A hautie looke, and a proude heart, which is the light of the wicked, is sinne.
5 Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
The thoughtes of the diligent doe surely bring abundance: but whosoeuer is hastie, commeth surely to pouertie.
6 Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
The gathering of treasures by a deceitfull tongue is vanitie tossed to and from of them that seeke death.
7 Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
The robberie of the wicked shall destroy them: for they haue refused to execute iudgement.
8 Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
The way of some is peruerted and strange: but of the pure man, his worke is right.
9 Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
It is better to dwell in a corner of the house top, then with a contentious woman in a wide house.
10 Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
The soule of the wicked wisheth euill: and his neighbour hath no fauour in his eyes.
11 Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
When the scorner is punished, the foolish is wise: and when one instructeth the wise, he wil receiue knowledge.
12 Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
The righteous teacheth the house of the wicked: but God ouerthroweth the wicked for their euill.
13 Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
He that stoppeth his eare at the crying of the poore, he shall also cry and not be heard.
14 Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
A gift in secret pacifieth anger, and a gift in the bosome great wrath.
15 Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
It is ioye to the iust to doe iudgement: but destruction shalbe to the workers of iniquitie.
16 Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
A man that wandreth out of the way of wisdome, shall remaine in the congregation of the dead.
17 Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
Hee that loueth pastime, shalbe a poore man: and he that loueth wine and oyle, shall not be riche.
18 Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
The wicked shalbe a ransome for the iust, and the transgressour for the righteous.
19 Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
It is better to dwell in the wildernesse, then with a contentious and angry woman.
20 Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
In the house of the wise is a pleasant treasure and oyle: but a foolish man deuoureth it.
21 Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
He that followeth after righteousnes and mercy, shall finde life, righteousnes, and glory.
22 Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
A wise man goeth vp into the citie of the mightie, and casteth downe the strength of the confidence thereof.
23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
He that keepeth his mouth and his tongue, keepeth his soule from afflictions.
24 Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
Proude, hautie and scornefull is his name that worketh in his arrogancie wrath.
25 Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
The desire of the slouthfull slayeth him: for his hands refuse to worke.
26 Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
He coueteth euermore greedily, but the righteous giueth and spareth not.
27 Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
The sacrifice of the wicked is an abomination: how much more when he bringeth it with a wicked minde?
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
A false witnes shall perish: but hee that heareth, speaketh continually.
29 Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
A wicked man hardeneth his face: but the iust, he will direct his way.
30 Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
There is no wisedome, neither vnderstanding, nor counsell against the Lord.
31 Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.
The horse is prepared against the day of battell: but saluation is of the Lord.

< Mithali 21 >