< Mithali 20 >

1 Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
El vino hace tontos a los hombres, y la bebida fuerte hace que los hombres lleguen a los golpes; y quien entra en error por esto no es sabio.
2 Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
La ira de un rey es como el fuerte grito de un león; el que lo enoja hace lo malo contra sí mismo.
3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
Es un honor para un hombre evitar pelear, pero los tontos siempre están en guerra.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
El que odia el trabajo no ara su arado debido al invierno; entonces, en el momento de cortar el grano, él estará pidiendo comida y no obtendrá nada.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
El propósito en el corazón de un hombre es como aguas profundas, pero un hombre con buen sentido lo sacará.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
La mayoría de los hombres no ocultan sus actos bondadosos, pero ¿dónde se puede ver a un hombre de buena fe?
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
Un hombre recto continúa con su justicia: ¡Felices son sus hijos después de él!
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
Un rey en el tribunal juzga todo el mal con sus ojos.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
¿Quién puede decir: Yo he limpiado mi corazón, estoy libre de mi pecado?
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
Pesas desiguales y medidas desiguales, todos son repugnantes para el Señor.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
Incluso un niño puede ser juzgado por sus obras, si su trabajo es libre de pecado y si es correcto.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
El oído que oye y el ojo que ve son igualmente obra del Señor.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
No seas amante del sueño, o llegarás a ser pobre: ​​mantén tus ojos abiertos, y tendrás suficiente pan.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
Malo, muy malo, dice él que está dando dinero por bienes; pero cuando ha seguido su camino, deja en claro su orgullo por lo que compró.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
Hay oro y una tienda de corales, pero los labios del conocimiento son una joya de gran precio.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
Toma prenda de un hombre si se hace responsable de un hombre extraño, y toma promesa de él que da su palabra por hombres extraños.
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
El pan de engaño es dulce para el hombre; pero después, su boca estará llena de arena.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
Todo propósito se lleva a cabo mediante la ayuda sabia: y guiando sabiamente la guerra.
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
El que habla acerca de los negocios de los demás revela secretos: así que no tengas nada que ver con el que tiene los labios abiertos de par en par.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
Si alguno maldice a su padre o a su madre, su luz se apagará en la noche más negra.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
Una herencia se puede obtener rápidamente al principio, pero el final no será una bendición.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
No digas: Daré castigo por el mal: sigue esperando al Señor, y él será tu salvador.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
Las pesas desiguales son repugnantes para el Señor, y las escalas falsas no son buenas.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
Los pasos de un hombre son del Señor; ¿cómo puede entonces un hombre tener conocimiento de su camino?
25 Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
Es un peligro para un hombre decir sin pensar, es santo y, después de tomar su juramento, cuestionarse si es necesario guardarlo.
26 Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
Un rey sabio echa a los malhechores y hace que su maldad vuelva a ellos.
27 Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
El Señor vela por el espíritu del hombre, buscando en todas las partes más profundas del cuerpo.
28 Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
La misericordia y la buena fe protegen al rey, y la sede de su poder se basa en actos rectos.
29 Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
La gloria de los jóvenes es su fuerza, y el honor de los viejos es su canas.
30 Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.
Por las heridas de la vara, el mal se va, y los golpes limpian las partes más profundas del cuerpo.

< Mithali 20 >