< Mithali 20 >
1 Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
El vino es un burlador y la cerveza es un pendenciero. Quien se deja llevar por ellos no es sabio.
2 Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
El terror de un rey es como el rugido de un león. Quien lo provoque a la ira perderá su propia vida.
3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
Es un honor para un hombre mantenerse alejado de las disputas, pero todos los tontos se pelearán.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
El perezoso no arará a causa del invierno; por lo que mendigará en la cosecha, y no tendrá nada.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
El consejo en el corazón del hombre es como las aguas profundas, pero un hombre comprensivo lo sacará.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
Muchos hombres pretenden ser hombres de amor indefectible, pero ¿quién puede encontrar un hombre fiel?
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
El hombre justo camina con integridad. Benditos sean sus hijos después de él.
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
Un rey que se sienta en el trono del juicio dispersa todo el mal con sus ojos.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
¿Quién puede decir: “He purificado mi corazón”? Estoy limpio y sin pecado”.
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
Pesos y medidas diferentes, ambos por igual son una abominación para Yahvé.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
Hasta un niño se da a conocer por sus actos, si su trabajo es puro, y si es correcto.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
El oído que oye y el ojo que ve, Yahvé ha hecho incluso a los dos.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
No ames el sueño, no sea que llegues a la pobreza. Abre los ojos y te saciarás de pan.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
“No es bueno, no es bueno”, dice el comprador; pero cuando se va por su camino, entonces se jacta.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
Hay oro y abundancia de rubíes, pero los labios del conocimiento son una joya rara.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
Toma la prenda de quien pone una garantía para un extranjero; y lo tienen en prenda por una mujer descarriada.
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
La comida fraudulenta es dulce para el hombre, pero después se le llena la boca de grava.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
Los planes se establecen mediante asesoramiento; ¡con una guía sabia haces la guerra!
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
El que va de un lado a otro como portador de cuentos revela secretos; por tanto, no te hagas compañía de quien abre mucho los labios.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
El que maldiga a su padre o a su madre, su lámpara se apagará en la oscuridad de las tinieblas.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
Una herencia ganada rápidamente al principio no será bendecido al final.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
No digas: “Pagaré el mal”. Espera a Yahvé, y él te salvará.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
Yahvé detesta las diferencias de peso, y las balanzas deshonestas no son agradables.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
Los pasos del hombre son de Yahvé; ¿cómo puede entonces el hombre entender su camino?
25 Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
Es una trampa para el hombre hacer una entrega precipitada, para luego considerar sus votos.
26 Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
Un rey sabio selecciona a los malvados, y conduce el trillo sobre ellos.
27 Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
El espíritu del hombre es la lámpara de Yahvé, buscando en todas sus partes más íntimas.
28 Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
El amor y la fidelidad mantienen al rey a salvo. Su trono se sustenta en el amor.
29 Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
La gloria de los jóvenes es su fuerza. El esplendor de los ancianos son sus canas.
30 Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.
Los golpes que hieren limpian el mal, y los golpes purgan las partes más íntimas.