< Mithali 20 >
1 Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
C’est une chose luxurieuse que le vin; et l’ivresse est tumultueuse: quiconque y met son plaisir ne sera pas sage.
2 Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
Comme le rugissement du lion, ainsi est la terreur du roi: celui qui le provoque pèche contre son âme.
3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
C’est un honneur pour l’homme, de se séparer des contestations; mais tous les insensés s’immiscent dans des affaires ignominieuses.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
À cause du froid, le paresseux n’a pas voulu labourer; il mendiera donc pendant l’été, et il ne lui sera rien donné.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
Comme une eau profonde, ainsi est le conseil dans le cœur de l’homme; mais l’homme sage l’épuisera.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
Beaucoup d’hommes sont appelés miséricordieux; mais un homme fidèle, qui le trouvera?
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
Le juste qui marche dans sa simplicité laissera après lui des enfants bienheureux.
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
Le roi qui est assis sur le trône de la justice dissipe tout le mal par son regard.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
Qui peut dire: Mon cœur est pur, je suis pur de péché?
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
Un poids et un poids, une mesure et une mesure, l’un et l’autre sont abominables auprès de Dieu.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
Par ses inclinations un enfant est connu: si ses œuvres sont pures et droites.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
L’oreille qui entend et l’œil qui voit, le Seigneur a fait l’un et l’autre.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
N’aime pas le sommeil, de peur que la détresse ne t’accable; ouvre les yeux et rassasie-toi de pain.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
C’est mauvais, c’est mauvais, dit tout acheteur; et après qu’il se sera retiré, alors il se glorifiera.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
Il y a de l’or et une multitude de pierreries; mais c’est un vase précieux que les lèvres savantes.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
Prends le vêtement de celui qui s’est fait caution pour un étranger; et parce qu’il a répondu pour des étrangers, emporte un gage de lui.
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
Un pain de mensonge est doux à l’homme; mais, ensuite, sa bouche sera remplie de gravier.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
Les pensées s’affermissent par les conseils, et c’est par de sages directions que doivent être conduites les guerres.
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
Quant à celui qui révèle les secrets, qui marche frauduleusement, et qui dilate ses lèvres, ne te lie pas avec lui.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
Celui qui maudit son père et sa mère, sa lampe s’éteindra au milieu des ténèbres.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
L’héritage vers lequel on se précipite dès le premier instant sera à la fin privé de bénédiction.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
Ne dis point: Je rendrai le mal; attends le Seigneur, et il te délivrera.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
C’est une abomination auprès du Seigneur, qu’un poids et un poids: la balance trompeuse n’est pas bonne.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
Par le Seigneur sont dirigés les pas de l’homme; mais qui des hommes peut comprendre sa voie?
25 Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
C’est une ruine pour l’homme de dévorer les saints, et après des vœux, de se rétracter.
26 Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
Un roi sage dissipe les impies, et courbe sur eux un arc de triomphe.
27 Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
Le souffle de l’homme est une lampe du Seigneur, laquelle découvre les parties intimes du corps.
28 Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
La miséricorde et la vérité gardent le roi, et par la clémence est affermi son trône.
29 Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
La joie des jeunes hommes, c’est leur force; et la dignité des vieillards, les cheveux blancs.
30 Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.
La lividité d’une blessure fera disparaître le mal; et les plaies dans les parties les plus intimes du corps le feront disparaître aussi.