< Mithali 20 >
1 Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
Le vin est déréglé, et l'ivresse insolente; l'insensé se laisse prendre dans leurs filets;
2 Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
La menace d'un roi ne diffère point de la colère du lion; celui qui le provoque pèche contre sa propre vie.
3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
C'est une gloire pour un homme de se détourner des contestations; au contraire, le fou s'y laisse prendre.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
Le paresseux, quand on le blâme, n'en a point honte; il en est de même de celui qui emprunte du blé à usure pendant la moisson.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
Le conseil dans le cœur de l'homme est une eau profonde; l'homme prudent y saura puiser.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
Un homme est une grande chose; un homme miséricordieux est un trésor; mais un homme fidèle est difficile à trouver.
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
L'homme irréprochable qui se tourne vers la justice laissera ses enfants heureux.
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
Lorsqu'un roi juste s'est assis sur son trône, nul mal ne résiste à ses regards.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
Qui peut se vanter d'avoir le cœur chaste? Qui osera dire: Je suis pur de tout péché?
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
Avoir deux poids et deux mesures, et en faire usage: deux choses infâmes devant le Seigneur.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
Le jeune homme en compagnie d'un saint sera réservé dans ses mœurs, et sa voie sera droite.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
L'oreille entend, et l'œil voit; l'un et l'autre sont l'œuvre du Seigneur.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
Ne te plais pas à médire, si tu ne veux être chassé. Ouvre les yeux, et rassasie-toi de pain.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
La lampe de celui qui décrie son père ou sa mère s'éteindra; les prunelles de ses yeux verront les ténèbres.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
Le bien acquis tout d'abord à la hâte, à la fin ne sera pas béni.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
Garde-toi de dire: Je me vengerai de mon ennemi; mais attends le Seigneur, afin qu'Il te seconde.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
Le double poids est en abomination au Seigneur, et les fausses balances ne sont point bonnes à Ses yeux.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
La marche d'un homme est maintenue droite par le Seigneur; car comment un mortel discernerait-il ses voies?
25 Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
L'homme tombe dans un piège, quand il se hâte trop de consacrer ses biens; car après le vœu vient le repentir.
26 Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
Un roi sage est le vanneur des impies, et il fait passer sur eux une roue.
27 Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
L'esprit de l'homme est une lumière du Seigneur, qui éclaire jusqu'au fonds des entrailles.
28 Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
La miséricorde et la vérité sont la garde du roi, et avec la justice elles font cercle autour de son trône.
29 Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
L'ornement des jeunes gens c'est la sagesse; la parure des vieillards, ce sont leurs cheveux qui grisonnent.
30 Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.
Les confusions et les blessures sont le partage des méchants; ils ont des plaies jusqu'au fond des entrailles.