< Mithali 20 >

1 Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
Wine [is] a scorner—strong drink [is] noisy, And any going astray in it is not wise.
2 Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
The fear of a king [is] a growl as of a young lion, He who is causing him to be angry is wronging his soul.
3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
Cessation from strife is an honor to a man, And every fool interferes.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
The slothful does not plow because of winter, He asks in harvest, and there is nothing.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
Counsel in the heart of a man [is] deep water, And a man of understanding draws it up.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
A multitude of men each proclaim his kindness, And a man of steadfastness who finds?
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
The righteous is habitually walking in his integrity, O the blessedness of his sons after him!
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
A king sitting on a throne of judgment, Is scattering all evil with his eyes,
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
Who says, “I have purified my heart, I have been cleansed from my sin?”
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
A stone and a stone, an ephah and an ephah, Even both of them [are] an abomination to YHWH.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
Even by his actions a youth makes himself known, Whether his work is pure or upright.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
A hearing ear, and a seeing eye—YHWH has even made both of them.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
Do not love sleep, lest you become poor, Open your eyes—be satisfied [with] bread.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
“Bad, bad,” says the buyer, And then he boasts himself going his way.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
Substance, gold, and a multitude of rubies, Indeed, a precious vessel, [are] lips of knowledge.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
When a stranger has been guarantor, take his garment, And pledge it for strangers.
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
The bread of falsehood [is] sweet to a man, And afterward his mouth is filled [with] gravel.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
You establish purposes by counsel, And with plans you make war.
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
The busybody is a revealer of secret counsels, And do not make yourself guarantor for a deceiver [with] his lips.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
Whoever is vilifying his father and his mother, his lamp is extinguished in blackness of darkness.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
An inheritance gotten wrongly at first, Even its latter end is not blessed.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
Do not say, “I repay evil,” Wait for YHWH, and He delivers you.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
A stone and a stone [are] an abomination to YHWH, And balances of deceit [are] not good.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
The steps of a man [are] from YHWH, And man—how does he understand his way?
25 Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
A snare to a man [that] he has swallowed a holy thing, And to make inquiry after vows.
26 Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
A wise king is scattering the wicked, And turns the wheel back on them.
27 Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
The breath of man [is] a lamp of YHWH, Searching all the inner parts of the heart.
28 Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
Kindness and truth keep a king, And he has supported his throne by kindness.
29 Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
The beauty of young men is their strength, And the honor of old men is grey hairs.
30 Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.
Blows that wound cleanse away evil, Also the scourges of the inner parts of the heart!

< Mithali 20 >