< Mithali 20 >
1 Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
Wine is a mocker and strong drinke is raging: and whosoeuer is deceiued thereby, is not wise.
2 Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
The feare of the King is like the roaring of a lyon: hee that prouoketh him vnto anger, sinneth against his owne soule.
3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
It is a mans honour to cease from strife: but euery foole will be medling.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
The slouthfull will not plowe, because of winter: therefore shall he beg in sommer, but haue nothing.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
The counsell in the heart of man is like deepe waters: but a man that hath vnderstanding, will drawe it out.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
Many men wil boast, euery one of his owne goodnes: but who can finde a faithfull man?
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
He that walketh in his integritie, is iust: and blessed shall his children be after him.
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
A King that sitteth in the throne of iudgement, chaseth away all euill with his eyes.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
Who can say, I haue made mine heart cleane, I am cleane from my sinne?
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
Diuers weightes, and diuers measures, both these are euen abomination vnto the Lord.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
A childe also is knowen by his doings, whether his worke be pure and right.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
The Lord hath made both these, euen the eare to heare, and the eye to see.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
Loue not sleepe least thou come vnto pouertie: open thine eyes, and thou shalt be satisfied with bread.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
It is naught, it is naught, sayth the buyer: but when he is gone apart, he boasteth.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
There is golde, and a multitude of precious stones: but the lips of knowledge are a precious iewel.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
Take his garment, that is suretie for a stranger, and a pledge of him for the stranger.
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
The bread of deceit is sweete to a man: but afterward his mouth shalbe filled with grauel.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
Establish the thoughtes by counsell: and by counsell make warre.
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
He that goeth about as a slanderer, discouereth secrets: therefore meddle not with him that flattereth with his lips.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
He that curseth his father or his mother, his light shalbe put out in obscure darkenes.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
An heritage is hastely gotten at the beginning, but the end thereof shall not be blessed.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
Say not thou, I wil recompense euill: but waite vpon the Lord, and he shall saue thee.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
Diuers weightes are an abomination vnto the Lord, and deceitful balances are not good.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
The steps of man are ruled by the Lord: how can a man then vnderstand his owne way?
25 Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
It is a destruction for a man to deuoure that which is sanctified, and after the vowes to inquire.
26 Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
A wise King scattereth the wicked, and causeth the wheele to turne ouer them.
27 Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
The light of the Lord is the breath of man, and searcheth all the bowels of the belly.
28 Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
Mercie and trueth preserue the King: for his throne shall be established with mercie.
29 Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
The beautie of yong men is their strength, and the glory of the aged is the gray head.
30 Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.
The blewnes of the wound serueth to purge the euill, and the stripes within the bowels of the belly.